URAIS TANZANIA 2015:-Mke wa Magufuli awaliza walimu, wanafunzi Mbuyuni. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, July 19, 2015

URAIS TANZANIA 2015:-Mke wa Magufuli awaliza walimu, wanafunzi Mbuyuni.

Bi.Janeth Magufuli ( Pichani ) bado anasubiri miezi mitatu ya kampeni nzito za kumuwezesha mumewe kuingia kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, lakini walimu na wanafunzi wa Shule ya Msingi Mbuyuni tayari wanasikitika kumpoteza mwalimu huyo wa jiografia, historia na Tehama.

Mumewe, Dk John Pombe Magufuli amepitishwa zaidi ya wiki moja iliyopita kuwa mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, na hivyo atalazimika kupambana vikali na wagombea wa vyama vingine ili kujihakikishia anaingia Ikulu kuongoza Serikali ya Awamu ya Tano.

Iwapo Dk Magufuli atachaguliwa kuliongoza Taifa Oktoba 25,2015, Shule ya Mbuyuni itakuwa imeweka historia ya aina yake kwa kutoa wake wawili wa marais.

Bi.Salma Kikwete, mke wa Rais anayemaliza muda wake, pia alifundisha shule hiyo katika kipindi chake cha miaka 20 ya utumishi serikalini.

Lakini kitu kingine cha aina yake ni kwamba iwapo Dk Magufuli atakuwa Rais, maana yake mkewe ataingia kwenye kundi la wake za marais wawili wa nchi zilizo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao majina yao ni Janeth.

Mke wa Rais wa Uganda ni Janet Kataaha Museveni wakati mke wa Rais Paul Kagame wa Rwanda anaitwa Jeannette Kagame.BOFYA HAPA KUSOMA ZIAIDI....''


Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad