MKUTANO WA ACT WAZALENDO KASULU:-Wanachama 798 Wahamia wakitoka NCCR Mageuzi na Vyama vingine. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, July 23, 2015

MKUTANO WA ACT WAZALENDO KASULU:-Wanachama 798 Wahamia wakitoka NCCR Mageuzi na Vyama vingine.


Mkutano wa Chama cha ACT Wazalendo umefanyika Jumanne ya July 21, 2015 mjini Kasulu ,mkoani Kigoma ambapo pamoja na mambo mengine Wanachama 798 wa Chama cha NCCR Mageuzi wilayani Kasulu Mkoani Kigoma wamekihama Chama hicho na kujiunga na Chama cha ACT Wazalendo wakimfuata Mbunge wa Jimbo la Kasulu Mjini anayemaliza Muda wake Bw Moses Machali na Katibu wake Bw Elisha Kabezi.

Wanachama hao wamejiunga na ACT Wazalendo katika Mkutano wa hadhara wa ACT Wazalendo wilayani humo uliofanyika kwenye Viwanja vya Kiganamo kwa lengo la Kumpokea Bw Machali na kumkabidhi kadi ya Chama hicho .

Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe (kulia) akimtambulisha kwa wananchi mwanachama mpya wa chama hicho Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Kasulu, mkoani Kigoma Julai 21,2015.

Mbali na Bw Machali na Katibu wake kujiunga na ACT Wazalendo, pia yumo aliyekuwa Diwani wa Kata ya Ahsante Nyerere kwa Tiketi ya NCCR Mageuzi pamoja na aliyekuwa Diwani wa Kata ya Rungwe Mpya kwa muhula wa Mwaka 2005 hadi 2010.

Kati ya wanachama hao, 648 wanatoka chama cha NCCR Mageuzi huku wengine wakitoka kwenye Vyama vingine ikiwemo Chama cha Mapinduzi na kisha kujiunga na ACT Wazalendo... 

Habari kwa hisani ya Radio Kwizera FM.

Pichani juu na chini Msafara ukiendelea kuelekea uwanjani .



Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad