![]() |
|
Mechi ya watani Simba SC na Yanga SC.
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) itaanza September, 12,2015 badala ya Agosti 22,2015 ili kumpa Charles Mkwasa fursa ya kuendelea na program yake kuelekea mechi ya Taifa Stars dhidi ya Nigeria itakayochezwa Sept 5,2015. Mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) itakayozikutanisha Azam FC dhidi ya Yanga SC sasa itachezwa Agosti 22,2015 badala ya Agosti 15,2015. Ratiba ya Ligi Kuu iliyokuwa imeandaliwa, sasa inafanyiwa marekebisho kwa ajili ya tarehe mpya ya kuanza, ambapo pamoja na mambo mengine mechi sasa zitachezwa wikiendi na katikati ya wiki na wikiendi ya Octoba 25,2015 hakutakuwa na mechi kupisha Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge. Klabu za Ligi Kuu zimeandikiwa barua kujulishwa tarehe mpya ya kuanza Ligi, na dirisha la usajili linabaki kama lilivyo. Wamiliki wa viwanja vyenye upungufu wameandikiwa barua kutakiwa kurekebisha upungufu katika muda maalumu, vinginevyo havitaruhusiwa kutumika kwa ajili ya PL na FDL. Timu ya Madini ya Arusha imeruhusiwa kutumia Uwanja wa Nyerere uliopo Mbulu mkoani Manyara kwa mechi za SDL kwa masharti upungufu uliopo kwenye uwanja huo urekebishwe kwanza.
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Tuesday, July 21, 2015
Home
MICHEZO
LIGI KUU TANZANIA BARA 2015 / 2016:- Haya hapa Mabadiliko Mapya sasa kuanza September 12,2015.
LIGI KUU TANZANIA BARA 2015 / 2016:- Haya hapa Mabadiliko Mapya sasa kuanza September 12,2015.
Tags
# MICHEZO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.






No comments:
Post a Comment