KAGAME CUP 2015:-Yanga wameshindwa kutamba kwenye uwanja wa nyumbani baada ya kubanjuliwa na vigogo vya Kenya timu ya Gor Mahia. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, July 18, 2015

KAGAME CUP 2015:-Yanga wameshindwa kutamba kwenye uwanja wa nyumbani baada ya kubanjuliwa na vigogo vya Kenya timu ya Gor Mahia.

Mashabiki wa Gor Mahia wakiwa wanaisapoti timu yao kwa nguvu zote kwenye mchezo wa ufunguzi  wa michuano ya Kagame Cup uliopigwa leo Julai 18,2015 jioni kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mashabiki wa Yanga wakiwa hawana matumaini bada ya timu yao kufungwa goli la pili na timu ya Gor Mahia kwenye mchezo wa ufunguzi uwanja wa Taifa.

Yanga wameshindwa kutamba kwenye uwanja wa nyumbani baada ya kubanjuliwa na vigogo vya Kenya timu ya Gor Mahia kwenye mchezo wa ufunguzi wa michuano ya Kagame Cup uliopigwa leo Julai 18,2015 jioni kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,baada ya kufungwa mabao 2-1 na Gor Mahia ya Kenya katika mchezo wa Kundi A .

Kipigo cha Yanga SC leo kwa kiasi kikubwa kilichangiwa na kucheza pungufu kwa zaidi ya dakika 65, kufuatia mshambuliaji wake, Mzimbabwe Donald Ngoma kutolewa kwa kadi nyekundu mapema kipindi cha kwanza.

Kama kawaida ya Yanga na Simba, mashabiki wa Simba wakiiunga mkono timu ya Gor Mahia.

Mshambuliaji wa Yanga Donald Ngoma alitolewa nje kwa kadi nyekundu kipindi cha kwanza baada ya kumpiga kwa makusudi mchezaji wa Gor Mahia.
Yanga walitangulia kupata goli dakika ya nne kipindi cha kwanza kupitia kwa mshambuliaji wao mpya Donald Ngoma walie msajili kutoka klabu ya FC Platinum ya Zimbabwe lakini bao hilo halikuweza kudumu kwani Haruna Shakava aliisawazishia Gor Mahia goli hilo dakika ya 16 ya kipindi cha kwanza na timu hizo kwenda mapumziko zikiwa sare ya kufungana goli 1-1.

Michael Olunga aliifungia Gor Mahia goli la pili dakika ya 45 katika kipindi cha pili na kuipa ushindi timu yake dhidi ya Yanga, mabingwa wa Tanzania bara (Yanga) walijitahidi kutafuta goli la kusawazisha lakini mambo yalikuwa magumu kwa upande wao.

Nadir Haroub ‘Cannavaro’ alikosa mkwaju wa penati baada ya mlinzi wa Gor Mahia kuunawa mpira kwenye eneo la hatari wakati akiwa kwenye harakati za kuokoa shambulizi lililofanywa na Yanga wakati wakilisakama lango la Gor Mahia wakitafuta goli la kusawazisha.

Nao APR ya Rwanda imeanza vyema michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Al Shandy ya Sudan Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo wa Kundi C, bao pekee la APR lilifungwa na kiungo Bizimana Djihad, dakika ya 64 kwa shuti kali baada ya kupasua katikati ya Uwanja na baada ya kupata upenyo.


Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad