|
Washika bunduki wa London, Arsenal wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa Asia
Trophy baada ya kuichapa Everton mabao 3-1 katika mechi ya fainali iliyopigwa
leo Julai 18,2015.
Kocha mkuu wa Arsenal, Arsene Wenger alikuwa ametulia kwenye benchi huku
vijana wake wakionesha kiwango cha hali ya juu katika mechi hiyo ambayo ni
sehemu ya maandalizi ya msimu mpya.
Golikipa mpya wa Arsenal aliyesajiliwa kutoka Chelsea majira haya ya
kiangazi, Petr Cech amecheza mechi yake ya kwanza na kuokoa michomo ya hatari.
Magoli ya Arsenal yamefungwa na Theo Walcott (22), Saint Cazorla (58) na
Mesut Ozil (63).
Bao pekee la Everton limefungwa na Ross Barkley (76) .
|
No comments:
Post a Comment