CHADEMA :-Yawatambulisha rasmi Lembel na Bulaya huku ikiahidi kutangaza mgombea urais wa Ukawa wakati muafaka utakapowadia. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, July 22, 2015

CHADEMA :-Yawatambulisha rasmi Lembel na Bulaya huku ikiahidi kutangaza mgombea urais wa Ukawa wakati muafaka utakapowadia.

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk. Willibroad Slaa akiwa kwenye gari katika msafara wa mapokezi kwa ajili ya mkutano wa hadhara wa kuwatambulisha Mbunge wa Kahama, Bw.James Lembeli na Mbunge wa Viti Maalumu, Bi.Ester Bulaya waliohamia Chadema wakitokea CCM,mkutano huo umefanyika leo hii July 22, 2015 jijini Mwanza.


Mbunge wa Jimbo la Kahama, mkoani Shinyanga, Bw.James Lembeli (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Taifa, Bw.John Mnyika, wakiwapungia wananchi mikono walipokuwa kwenye msafara wa mapokezi ya Viongozi Wakuu wa Chama hicho wakiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya mkutano mkubwa wa hadhara.
Marafiki wawili, Mbunge wa Viti Maalumu, Bi.Ester Bulaya aliyehamia Chadema akitokea CCM ...... akifurahia jambo na Halima Mdee.
Pichani juu na chini Msafara ukiendelea kuelekea uwanjani .

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amewakabidhi rasmi kadi za uanachama, aliyekuwa Mbunge wa Kahama, Mh. James Daudi Lembeli (Pichani kulia ) na aliyekuwa Mbuge wa Kuteuliwa mkoani Mara, Ester Amos Bulaya kwenye Mkutano wa chama hicho unaoendelea mpaka sasa jijini Mwanza.
Mwenyekiti wa taifa wa Chadema Mh.Freeman Mbowe.

Chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) na vyama washirika vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA ) wamesema kuwa wako imara na wamejiandaa vyema kushinda katika uchaguzi mkuu ujao kwa kukiondoa madarakani chama cha mapinduzi, licha ya kauli inayodaiwa kutolewa na katibu mwenezi wa chama hicho Nape Nnauye wakati wa ziara ya katibu mkuu wa chama hicho mkoani Mwanza kwamba CCM itashinda hata kwa goli la mkono.

Kauli hiyo imetolewa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya magomeni kirumba jijiji Mwanza na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi wa mikoa ya kanda ya ziwa ambapo katika mkutano huo mwenyekiti wa taifa wa Chadema Mh.Freeman Mbowe amewatambulisha rasmi waliokuwa wabunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi Mh. James Lembeli na Mh. Esther Bulaya ambao wamehamia Chadema, huku akiwatahadhalisha wagombea wa nafasi za udiwani na ubunge kutokubali kununuliwa  kwa lengo la kukihujumu chama hicho.

Awali mwenyekiti wa taifa wa baraza la wanawake wa Chadema (BAWACHA) Halima Mdee, naibu katibu mkuu wa chama hicho upande wa Zanzibar Salum Mwalim pamoja na mwanasheria wa Chadema Tundu Lissu wamesema wakati umefika kwa watanzania kuchagua viongozi wanaokubalika na wenye uchungu na raslimali za taifa kwa uhuru bila kutishwa kwani saa ya ukombozi kupitia sanduku la kura utajulikana oktoba 25 mwaka huu.

Kwa upande wao waliokuwa wabunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi James Lembeli wa jimbo la Kahama na Esther Bulaya viti maalum umoja wa vijana CCM mkoa wa Mara nao wametumia mkutano huo kueleza kilichowasukuma kujiunga na Chadema.


Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad