CECAFA KAGAME CUP 2015:-Gor Mahia yaenda robo fainali baada ya kuitandika KMKM leo July 20, 2015. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, July 20, 2015

CECAFA KAGAME CUP 2015:-Gor Mahia yaenda robo fainali baada ya kuitandika KMKM leo July 20, 2015.

Mshambuliaji wa Kenya Michael Olunga amezidi kung’ara kwenye michuano ya Kagame Cup 2015 baada ya kufunga magoli mawili kwenye mchezo wa leo Julai 20,2015 uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa kati ya KMKM ya Zanzibar dhidi ya Gor Mahia ya Kenya.
Gor Mahia imekuwa timu ya kwanza kutinga kwenye hatua ya robo fainali kwenye michuano ya Kagame Cup 2015 baada ya kuibuka na ushindi kwenye michezo yake miwili kwenye Kundi A, kundi pekee lenye timu tano kwenye michuano ya Kagame. 

Gor Mahia waliibuka na ushindi wa goli 2-1 kwenye mchezo wao wa ufunguzi kwa kuifunga Yanga SC na leo Julai 20,2015 wameitwanga KMKM goli 3-1 na kuongoza Kundi A kwa kuwa na pointi sita huku wakiwa wamefunga magoli matano wakati wao wamefungwa magoli mawili kwenye mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.


 Katika Mechi hiyo, Gor Mahia walitangulia Dakika ya 3 tu kwa Bao la Meddie Kagere na KMKM kurudisha Dakika ya 12 kwa Bao  la Saimon.

Kipindi cha Pili, Nyota wa Gor Mahia Michael Olunga, aliipigia Timu yake Bao 2 na kuipa ushindi wa Bao 3-1.

Juzi, Gor Mahia ilianza Mechi zake za Kundi A kwa kuifunga Yanga Bao 2-1.

Katika Mechi nyingine ya Kundi A iliyochezwa mapema Leo, Al Khartoum ya Sudan iliitwanga Telecom ya Djibouti Bao 5-0.

Kesho ,Jumanne Julai 21,2015 zipo Mechi mbili za Kundi B kati ya Al Shandy na LLB AFC Saa 8 Mchana, Uwanja wa Taifa, na kufuatiwa na ile ya Hegaan vs  APR hapo Saa 10 Jioni huko Karume Stadium, wakati Mechi ya Kundi  C kati ya Malakia na Azam itachezwa Uwanja wa Taifa kuanzia Saa 10 Jioni.  

MSIMAMO KAGAME CUP  2015.

Kundi A

1- Gor Mahia (Kenya) Mechi 2 Magoli 5-2 Pointi 6

2- Khartoum (Sudan) Mechi 1 Magoli 5-0 Pointi 3 

3- KMKM (Zanzibar) Mechi 2 Magoli 2-3 Pointi 3

4- Yanga (Tanzania Bara) Mechi 1 Magoli 1-2 Pointi 0

5- Telecom (Djibout) Mechi 2 Magoli 0-6 Pointi 0

Kundi B

1- APR (Rwanda) Mechi 1 Magoli 1-0 Pointi 3

2- LLB AFC (Burundi) Mechi 1 Magoli 0-0 Pointi 1

3- Heegan  FC (Somalia) Mechi 1 Magoli 0-0 Pointi 1

4- Al Shandy (Sudan) Mechi 1 Magoli 0-1 Pointi 0

Kundi C

1- Malakia (Sudan Kusini) Mechi 1 Magoli 2-1 Pointi 3

2- Azam FC (Tanzania) Mechi 1 Magoli 1-0 Pointi 3

3- Adama City (Ethiopia) Mechi 1 Magoli 1-2 Pointi 0

4- KCCA (Uganda) Mechi 1 Magoli 0-1 Pointi 0

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad