ELIMU YETU:-Taswira Picha ya Mahafali ya Kidato cha Sita shule ya Sekondari Kabanga iliyopo wilayani Ngara Mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, May 01, 2015

ELIMU YETU:-Taswira Picha ya Mahafali ya Kidato cha Sita shule ya Sekondari Kabanga iliyopo wilayani Ngara Mkoani Kagera.


Wahitimu wa kidato cha sita Shule ya Sekondari Kabanga iliyopo wilayani Ngara mkoani Kagera wakiwa  katika mahafali yao ya tano katika shule hiyo  yaliyohusisha wahitimu 96 ambapo katika risala yao kwa Mgeni Rasmi Mkuu wa wilaya ya Ngara Bw. Costantine Kanyasu,walibainisha kuwa Upungufu wa mabweni ,vitabu vya kiada na ziada pamoja na walimu wa sayansi ni baadhi ya changamoto zinazowakabili wanafunzi wa shule hiyo katika mazingira ya kujifunzia

Mkuu wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera  Bw Costantine Kanyasu akigawa vyeti kwa wahitimu wa kidato cha sita ,katika shule ya sekondari Kabanga ambapo pamoja na mambo mengine amewataka watendaji wa vijiji na kata kuwakamata wazazi na walezi kisha kuwafikisha mahakamani wanaopuuzia kulipa karo na michango katika shule za sekondari na ukamataji wa wazazi hao uwe sambamba na wanafunzi walioacha shule kwa sababu tu za utoro bila kuwa na sababu za msingi kama sio utovu wa nidhamu.

Awali mkuu wa shule ya sekondari Kabanga wilayani Ngara Bw Aaron Dishon amesema wazazi wamekuwa kikwazo cha kuendeleza wanafunzi kitaaluma kwa kuchelewesha fedha za ada ikiwemo michango ya taaluma shuleni hapo.  

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad