MAAMUZI MAGUMU:-CCM kuwatosa wanaowania Urais?? - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, April 13, 2015

MAAMUZI MAGUMU:-CCM kuwatosa wanaowania Urais??

Chama cha Mapnduzi kimesema kipo tayari kuyaweka kapuni majina ya makada wake sita walioadhibiwa kwa kosa la kuanza kapeni  za kuwania Urais katika uchaguzi mkuu ujao (2015)kabla ya muda.

 Kimesema hatua hiyo itakuja kama haitapokea ripoti ya kamati ndogo ya nidhamu inayoongozwa na makamu Mwenyekiti wa chama hicho Philip Mangula kabla ya kumalizka kwa muda wa uteuzi.

Tamko hilo la CCM limetolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye katika mahojiano kuhusu hatma ya kifungo cha makada hao pamoja na msimamo wa chama kuhusu makada wake wengine wanaodaiwa kutenda kosa kama hilo.

Nape alisema kwa sasa kifungo cha makada hao hakifahamiki kitaisha lini na endapo watatupwa nje ya mbio za kuwnaia urais wanapaswa kijilaumu wenyewe kwa makosa yao ya kukiuka taratibu za chama.

Makada walio katika kifungo ni pamoja na Waziri mkuu wa zaman Edward Lowassa,Waziri wa mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe,Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika Stephen Wasira,Naibu Waziri wa Mawasiliano na teknolojia January Makamba na Mbunge wa Sengerema Willium Ngeleja.

Source:-Mtanzania.

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad