![]() |
|
Klabu ya
Simba SC leo April 6, 2015,imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 2-1 dhidi ya
wenyeji wao Kagera Sugar katika mtanange uliopigwa kwenye uwanja wa CCM Kambarage
mjini Shinyanga.
Simba SC ndio
walikuwa wa kwanza kupata bao kunako dakika ya 49 kipindi cha pili kupitia kwa
Ramadhan Singano kabla ya Kagera Sugar kusawazisha kupitia kwa Rashid Mandawa.
Mshambuliaji
wa Simba Ibrahim Ajib aliipachikia timu hiyo goli la pili na la ushindi kwa
mkwaju wa penati.
Ibrahim
Hajib aliifungia Simba SC bao la pili kwa penalti dakika ya 71, kufuatia Erick
Kyaruzi kuunawa mpira kwenye eneo la hatari katika harakati za kuokoa.
Hilo
linakuwa bao la 10 katika Ligi Kuu msimu huu kwa Mandawa, ambaye sasa
amemkamata mshambuliaji wa Azam FC, Didier Kavumbangu- wote wakiwa nyuma ya
winga wa Yanga SC, Simon Msuva anayeongoza kwa mabao yake 11.
Unaweza sema
Simba SC sasa wanafufua matumaini ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara msimu huu 2014/2015, kufuatia ushindi huo unaowafikisha pointi 35 baada ya kucheza
mechi 21, ikizidiwa pointi moja tu na mabingwa watetezi, Azam FC wenye pointi
36, lakini wamecheza mechi 18. Yanga SC wenye pointi 40 za mechi 19, wapo
kileleni.
|
Monday, April 06, 2015
Home
MICHEZO
LIGI KUU BARA 2014/2015:-Simba SC na Matumaini ya Ubingwa baada ya Kuifumua 2-1 Kagera Sugar.
LIGI KUU BARA 2014/2015:-Simba SC na Matumaini ya Ubingwa baada ya Kuifumua 2-1 Kagera Sugar.
Tags
# MICHEZO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.






No comments:
Post a Comment