KUTOA NI MOYO NASI UTAJIRI:-Msaada unahitajika kwa Mama huyu aliyejifungua mapacha 4. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, April 03, 2015

KUTOA NI MOYO NASI UTAJIRI:-Msaada unahitajika kwa Mama huyu aliyejifungua mapacha 4.

Mapacha wanne waliozaliwa jana katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma, Maweni.Kwa yeyote mwenye kuguswa na ana nia ya kumsaidia Zuwena Abdul, tafadhali wasiliana nae kwa namba za simu zifuatazo: 0759 558472.

Bi.Zuwena Abdul (29), Pichani ,Mkazi wa Buzebazeba, Manispaa ya Kigoma Ujiji, ambaye April 01,2015 alijifungua mapacha wanne katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma, Maweni, anaomba msaada kutoka kwa wasamaria wema, serikali na asasi mbali mbali za kijamii, ili aweze kuwatunza watoto wake mapacha wanne aliojifungua.

Zuwena anaomba msaada huo kutokana na kwamba hana kipato chochote kumudu kuwatunza watoto wake kwani yeye ni mama wa nyumbani  na mume wake Rajabu Mkangwa, anajishughulisha na shughuli ndogo ndogo za uzalishaji.

Ingawa amesema anajisikia faraja kujifungua mapacha hao, lakini changamoto iliyoko mbele yake ni namna ya kuwalea kutokana na familia yake kuishi maisha duni.

Mama mzazi wa Zuwena, Jaqlina Augustino, mkazi wa Gungu Manispaa ya Kigoma Ujiji, amesema uzazi wa mwanae wa kujifunga mapacha wanne uliwashitua mno, kwani licha ya familia za pande zote mbili, yaani upande wa Zuwena na ule wa mume wake kuwa na historia ya mapacha lakini haijawahi kutokea mtu kuzaa mapacha wanne.

Afisa Muuguzi Msaidizi katika Hospitali ya Maweni, Agnesi Nguvumali, alisema Zuwena alijifungua kwa njia ya kawaida mapacha wanne jana majira ya saa kumi na mbili jioni, ambao kati yao watatu ni wa kiume na mmoja wa kike,ambapo amesema kuwa mtoto wa kwanza amezaliwa akiwa na uzito wa kilo 1.8, wa pili kilo 2.5, wa tatu 1.7na wa nne kilo 1.7.

Tunawatunza kwa njia ambayo tunaita Kangaroo, kama ambavyo Kangaroo yule mnyama anavyotunza mtoto wake kifuani,”alisema Agnesi.

Alisema aina hiyo ya utunzaji kwa ngozi ya mama na mtoto kugusana, inamsaidia mtoto kupata uzito mkubwa kwa sababu ya joto la mama tofauti na njia zilizokuwa zikitumiwa hapo mwanzo ikiwemo ya kuvundika.

Kikubwa tunachoomba yule mama kama alivyosema ni mama wa nyumbani, angeweza kusaidiwa hasa kwenye maziwa ili aweze kutunza hawa watoto wakaweza kukua; kwa yeyote atakaeguswa aweze kumsaidia huyu mama,”aliongeza afisa muuguzi huyo.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma, Maweni, Fadhili Kibaya, alisema mpaka sasa hali za watoto hao pamoja na mama yao zinaendelea vizuri.

Kufuatia kujifungua mapacha hao wanne, Bi. Zuwena sasa amefikisha idadi ya watoto 8 kwani kabla ya mapacha hao yeye na mume wake tayari walikuwa na watoto wengine 4.

Kwa yeyote mwenye kuguswa na ana nia ya kumsaidia Zuwena Abdul, tafadhali wasiliana nae kwa namba za simu zifuatazo:- 0759 558472.


Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad