HABARI / PICHA:-Taswira ya Mgomo wa Madereva nchini Tanzania ilivyotikisa leo April 10, 2015 na Tamko la Serikali. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, April 10, 2015

HABARI / PICHA:-Taswira ya Mgomo wa Madereva nchini Tanzania ilivyotikisa leo April 10, 2015 na Tamko la Serikali.


Mabasi yaendayo mikoani yakiwa Stendi ya Ubungo yamepaki kufuatia mgomo wa Madereva nchini Tanzania kupinga agizo la Mamlaka ya Kudhibiti Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) lililowataka kwenda kusoma katika Chuo cha Usafirishaji (NIT).


Aidha Serikali tayari pamoja na madereva wamekubaliana kukutana Aprili 18 mwaka huu 2015 kwa ajili ya kuzungumza njia mbadala ambayo inaweza kuwasaidia katika kutatua tatizo hilo.

Tamko hilo limetolewa na  Waziri wa Kazi na Ajira, Mhe. Gaudencia Kabaka la kufuta agizo lililokuwa likiwataka madereva wa mabasi na malori kwenda kusoma katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) limesababisha madereva waliogoma kusafirisha abiria kwenye daladala kuanza kazi za kusafirisha abiria leo mchana.

Waziri Kabaka alisema mchana wa leo kwamba serikali Waziri alilitaka jeshi la polisi nao kuondoa tochi za barabarani ambazo zilikuwa moja ya kero ya madereva barabarani.



Hali halisi ya Ubungo ilivyokuwa asubuhi leo April 10, 2015.


Umati wa watu ukimshuhudia jamaa mmoja aliyekuwa akitoa ibada fupi ya kuombea nchi kuhusiana na mgomo wa madereva ambao ni wa nchi nzima eneo la Ubungo.

MADEREVA wa mabasi ya mikoani na daladala wa jijini Dar es Salaam leo April 10,2015 wamefanya mgomo kupinga agizo la Mamlaka ya Kudhibiti Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) lililowataka kwenda kusoma katika Chuo cha Usafirishaji (NIT).

Mwandishi wetu pia aliweza kufika eneo la Stendi ya Ubungo na kujionea hali ilivyokuwa asubuhi na kuzungumza na baadhi ya madereva ambao walikuwa na kauli tofautitofati kuhusiana na mgomo huo.

Mmoja wa madereva ambaye alijitambulisha kwa jina la Ally Abdallah Shalon anayefanya kazi zake kati ya Dar es Salaam na Dodoma, alisema kuwa sababu kubwa ya kutokufanya shughuli zake ni kutokana na kikao ambacho walipanga kukifanya leo kujadili agizo la Sumatra lililowataka waende shule kusoma.

Dereva mwingine aliyejitambulisha kwa jina moja la Khamis anayefanya shughuli zake kati ya Mwanza na Dar es Salaam alisema sababu iliyomfanya agome ni kupinga sheria mpya ya Sumatra iliyopitishwa na jeshi la polisi kuwataka madereva wote wa abiria (Pasangers Services Vehicle) kwenda kusoma kozi ya miezi miwili kwa gharama ya shilingi laki tano.

Khamisi alisema sheria hiyo inawabana sana madereva kwani moja kati ya vipengele vya sheria hiyo imeeleza kuwa, dereva yeyote atakayekamatwa akiwa amezidisha mwendo kasi hakuna faini yoyote bali unapelekwa mahabusu kwa muda wa siku kumi na nne baada ya kumaliza siku hizo, anapelekwa mahakamani kujibu shitaka linalomkabili.

Hii sheria inatubana sana, mtu ukihitaji kubadilisha leseni yako ikipitwa na muda unatakiwa kurudia tena kwenda kusoma darasani kwa muda wa wiki mbili kwa ada isiyopungua laki tano na kuendelea kitu ambacho kinatuumiza sisi madereva,” alisema Khamis.

MUSOMA

Huko Musoma, abiria zaidi 1000 waliokuwa wakisafiri kutoka Musoma kwenda Dar es Salaam kupitia mkoani Mwanza na Shinyanga na wale wa kwenda mpakani mwa Tanzania na Kenya pamoja na wa ndani ya Mkoa wa Mara wameshindwa kusafiri baada ya madareva kuitisha mgomo leo.

KIBAHA

Zaidi ya mabasi 10 kutoka mikoa ya kanda ya ziwa yamekwama huko Kibaha mkoani Pwani kutokana na mgomo wa madereva leo.

BUKOBA

Mabasi yote ya abiria yaliyotoka Bukoba Mjini leo asubuhi kuelekea Dar, Mwanza na kwingineko yamezuiliwa wilayani Muleba kutokana na mgomo wa madereva unaoendelea nchini kote. Abiria wamerudi mjini Bukoba kurudishiwa nauli zao na kuahirisha safari.

(PICHA/HABARI: DENIS MTIMA/GPL)


Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
  


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad