![]() |
|
Taarifa za uhakika zinasema watu watano (5) akiwemo kiongozi wa
Simba Ukawa, Mohammed Kingolile ‘Ngumi Jiwe’ wamefariki dunia na watu 15 wapo
mahututi na wamelazwa katika Hosptali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro wakipatiwa Matibabu.
Ajali hiyo imetokea eneo la Mvomero ikihusisha basi dogo aina ya Toyota Costa lililopinduka na kuacha njia. Polisi bado hawajatoa tamko rasmi.
Waliotangulia mbele ya haki mpaka sasa ni:-,Waluya, Rehema, Ali Kingolile ‘Ngumi Jiwe’ Wabi na dereva wa
gari Abdallah Fundi.
Simba SC,
mabingwa mara 18 wa Tanzania Bara, watakuwa na kazi ngumu ya kupata pointi
dhidi ya kikosi shadidi cha Kagera Sugar katika mechi yao ya kesho usukumani
Uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga.
Kagera Sugar
FC, mabingwa wa Kombe la Tusker 2004, waliifunga Simba SC bao 1-0 Uwanja wa
Taifa jijini hapa Novemba mwaka jana. Shukrani kwa bao la Atupele Green
lililokumbusha uchungu wa sare ya 1-1 ya msimu uliopita wa ligi iliyowachefua
baadhi ya mashabiki wa Simba SC waliokwaza na refa Mohamed Teofile wa Morogoro
baada ya kuipa tuta la dakika za mwisho lililopia sare timu hiyo ya Kagera.
Baada ya
kucheza mechi 20, Simba iko nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi ikiwa na
pointi 32, nane nyuma ya vinara Yanga SC na tano mbele ya Kagera Sugar FC
walioko nafasi ya nne baada ya mechi 20 pia.
Mechi
6 za Simba zilizobaki ni:-
Kagera Sugar FC vs Simba SC Simba SC vs Mgambo Shooting Mbeya City FC vs Simba SC Simba SC vs Ndanda FC Simba SC vs Azam FC
JKT Ruvu vs
Simba SC
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila tukio/stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Friday, April 03, 2015
Home
MATUKIO
HABARI MBAYA:-Mashabiki Watano wa Simba SC wapata ajali ya gari leo April 3, 2015 mkoani Morogoro.
HABARI MBAYA:-Mashabiki Watano wa Simba SC wapata ajali ya gari leo April 3, 2015 mkoani Morogoro.
Tags
# MATUKIO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MATUKIO
Labels:
MATUKIO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.







No comments:
Post a Comment