ELIMU YETU:-Redio za jamii zashukuru kwa kupokea Katiba Inayopendekezwa kwa njia ya Sauti. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, April 09, 2015

ELIMU YETU:-Redio za jamii zashukuru kwa kupokea Katiba Inayopendekezwa kwa njia ya Sauti.

Wasimamizi wa Redio za Jamii wakisikiliza kwa makini wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Mtandao wa redio za Jamii, Joseph Sekiku akiongea machache kabla ya kuwagawia wasimamizi wa redio za jamii wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO nchini Tanzania Bi. Zulmira Rodrigues, akiwagawia wasimamizi wa redio za jamii katiba iliyopendekezwa iliwekwa kwa njia ya sauti.

Wakurugenzi na Viongozi mbalimbali wa Radio za Jamii wamethibitisha kupokea na kuanza kurusha Katiba Inayopendekezwa kwa njia ya sauti, makala na michezo ya radio iliyoandaliwa na Kampuni ya Focus Media na COMNETA zenye maudhui ya katiba inayopendekezwa.

Wakizungumza na Focus Media ambao ndio waandaaji na wasambazaji wamekiri kwamba wamepokea kwa wakati muafaka, kwani hawakuwa na chanzo sahihi cha kupata maudhui yanayohusu elimu ya uraia na uchaguzi mkuu na kura ya maoni.

Baadhi ya wasimamizi wa Radio zilizo katika mtandao wa radio za kijamii Community Media Network of Tanzania ambao wamethibitisha kupokea vitendea kazi hivyo ni Bw. Ali Khamis Mtwana, Mkurugenzi Mtendaji wa Tumbatu Island Community Radio, Bw. Anton Masai Triple A FM Arusha, Dr. Lazaro Ole Mongoi Mkurugenzi Mtendaji wa IDEA Radio, Henry Bernard, Adelina Lweramla, Jackson Mollel, wa ORS FM Arusha, Edwin Mpokasye, Radio Fadhila, Mkurugenzi Radio Kwizera- Ngara.

Vipindi vinapokuwa vikiruka hewani wasikilizaji wamekuwa wakishiriki kwa kupiga simu na kuuliza maswali ilikuelewa zaidi Katiba Inayopendekezwa.

Wengine wanapiga simu kupongeza na mnamichezo ya radio ilivyoratibiwa vizuri na ikielimisha jamii juu ya mambo mbalimbali muhimu.

Source:-Dewji Blog


ILI KUSIKILIZA VIPINDI HIVI VYENYE MAUDHUI YA KATIBA INAYOPENDEKEZWA TEMBELEA.

http://myradiostream.com/focusradiotz

www.katibainayopendekezwa.or.tz

www.facebook.com/KatibaInayopendekezwaTanzania

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
 


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad