![]() |
...Komba
enzi za uhai wake.
Kapteni
Komba ambaye pia ni Mkurugugenzi wa Kikundi cha Maigizo cha Tanzania One
Theatre (TOT), ambacho kina kikundi cha taarabu na bendi
inayokwenda na mtindo wa Achimenengule, amekuwa akikisaidia sana chama chake,
Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kampeni zake wakati wa uchaguzi kwa kutunga
nyimbo za kuhamasisha wapiga kura na kushiriki kupiga live kwenye majukwaa ya
kisiasa.
Enzi za uhai
wake alitamani sana na kufanya juhudi kubwa ili mtindo wa Achimenengule
uwe wa kitaifa lakini ikashindikana, na badala yake Watanzania sasa tuna
muziki wa Mduara ambao umekuwa kama mtindo wa muziki wetu kwa sababu zifuatazo.
Kwanza, ni
mtindo halisi wa Kitanzania uliochipuka kutoka mahadhi ya kimwambao ya
Tanzania. Pili, ndiyo mtindo pekee uliowahi kutumiwa na bendi nyingi baada ya
kuasisiwa na ‘mabingwa’ wa muziki wetu, wana Njenje, The Kilimanjaro Band.
Baada ya
bendi hiyo kuuasisi, mtindo huo, tayari umepigwa na bendi kama TOT Plus, Chuchu
Sound, Pamo Sound, Inafrika Band, wana mipasho kadhaa na mwanamuziki mahiri
lakini asiyethamini kiwango chake kikubwa cha muziki, Bob Haisa.
Sababu ya
tatu ni kwamba mtindo huo umekuwa wa kupigwa na bendi nyingi, vikundi vingi na
wanamuziki wengi si kwa kulazimisha bali kwa mapenzi tu ya mashabiki wa muziki
wa Tanzania.
Kapteni
Komba awali alikuwa mwalimu wa shule ya msingi kabla ya kuingia jeshini na kuwa
kiongozi wa kikundi cha maonesho cha jeshi na baadaye Rais Mstaafu Ali Hassan
Mwinyi akamshawishi aachane na jeshi na kujiunga na CCM wakati wa mfumo wa
vyama mingi ulipoingizwa mwaka 1992.
“Mzee Mwinyi
ndiye aliyenifanya niache jeshi wakati huo nikiwa na cheo cha ukapteni.
Aliniomba nikisaidie chama kwa kuanzisha kikundi ambacho lengo lake lilikuwa
kukipigia debe CCM,” aliwahi kusema hivyo Kapteni Komba.
Ameshiriki
kampenzi za marais Ally Hassan Mwinyi, Benjamin William Mkapa na aliye
madarakani hivi sasa, Jakaya Mrisho Kikwete. Alikuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu
ya CCM Taifa na Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi hadi kifo kinamchukua.
Licha ya
siasa Kapteni Komba alikuwa anamiliki shule na pia alikuwa na biashara kadhaa.
Mwaka 2012 Komba aliwahi kupelekwa India kwa matibabu ambapo alifanyiwa upasuaji wa nyonga baada ya kupata ugonjwa uliosababisha mifupa kusagana sehemu hiyo ya nyonga.
Baada ya
kurejea nchini alisema upasuaji huo ulichukua saa tano na ulifanyika katika
Hospitali ya Apollo, India na alikanusha kuwa alikuwa na ugonjwa wa
figo.Ugonjwa uliomuua haujajulikana ila mtandao huu unafuatilia kila hatua na
utakujuza.
Marehemu
Komba ameacha mjane, Bi Salome, ambaye ni mwalimu kitaalumu na watoto kadhaa.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi- ameen!
UNGANA NASI KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Saturday, February 28, 2015

TANZIA:- Undani wa Kifo cha Mbunge JOHN KOMBA Aliefariki Dunia leo Februari 28,2015.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment