Wachezaji wa
Yanga wakishangilia bao lao dhidi ya BDF katika mchezo wa jana lililofungwa na
Mrisho Ngassa dhidi ya BDF wa Kombe la Shirikisho barani Afrika uliochezwa jana
mjini Gaborone, Botswana. BDF ilishinda mabao 2-1. Picha na Khatimu Naheka
.
Huko
Gaborone, Botswana hapo Jana Februari 27,2015, Yanga ilifungwa Bao 2-1 na BDF
XI kwenye Mechi ya Pili ya Raundi ya Awali ya Mashindano ya CAF ya Kombe la
Shirikisho lakini wamesonga na kutinga Raundi ya Kwanza kwa Jumla ya Mabao 3-2
baada ya kushinda Mechi ya Kwanza 2-0 Mjini Dar es Salaa.
Kwenye Mechi
ya Jana, Yanga walitangulia Bao 1-0 hadi Mapumziko alilofunga Mrisho Ngassa
lakini BDF XI Kipindi cha Pili walifunga Bao 2 na Gemu kwisha 2-1 huku Yanga pa
wakiwa Mtu 10 baada ya Danny Mrwanda kupewa Kadi Nyekundu katika Dakika ya 70.
BDF XI pia
walicheza Mtu 10 kuanzia Dakika ya 21 baada ya Mchezaji wao Mparithe kutolewa
kwa Kadi Nyekundu.
Katika
Raundi ijayo, Yanga watacheza na Mshindi kati ya Platinum ya Zimbabwe na
Sofapaka ya Kenya ambao wanarudiana Wikiendi hii huku Platinum wakiwa washindi
wa Bao 2-1 katika Mechi ya Kwanza iliyochezwa Nairobi.
Leo,Jumamosi Februari 28,2015, Timu
nyingine mbili za Tanzania, Azam FC na KMKM, zitakuwa Viwanjani kwenye Mechi
zao za Pili za Raundi ya Awali ya CAF CHAMPIONS LIGI wakati Polisi ya Zanzibar
itacheza Mechi yake ya Pili ya Raundi ya Awali ya Mashindano ya CAF ya Kombe la
Shirikisho hapo Jumapili.
MICHUANO
KLABU AFRIKA.
Raundi ya
Awali-Mechi za Marudiano
**Kwenye
Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza
CAF
CHAMPIONZ LIGI
Jumamosi
Februari 28,2015.
El Merreikh
[Sudan] v Azam FC [0-2]
KMKM v Al
Hilal [Sudan] [0-2]
CAF KOMBE LA SHIRIKISHO.
Ijumaa
Februari 27,2015.
BDF IX 2
Yanga 1 [2-3] === Yanga SC imesonga
Jumapili
Machi 1,2015.
Polisi v CF
Mounana [Gabon] [0-5]
Azam FC
wanahitaji Sare, au hata kufuungwa Bao 1-0, ili kusonga, Timu za Zanzibar, KMKM
na Polisi, zinahitaji ushindi mzito ili kupindua matokeo mabaya ya Mechi zao za
kwanza walizocheza Ugenini.
UNGANA NASI KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Saturday, February 28, 2015
Home
MICHEZO
CAF KOMBE LA SHIRIKISHO.:-Yanga SC yasonga mbele,watacheza na Mshindi kati ya Platinum au Sofapaka .
CAF KOMBE LA SHIRIKISHO.:-Yanga SC yasonga mbele,watacheza na Mshindi kati ya Platinum au Sofapaka .
Tags
# MICHEZO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment