Bondia nyota
nchini, Francis Cheka ‘SMG’ amehukumiwa miaka mitatu jela katika Mahakama ya
mkoani Morogoro leo Februari 02,2015.
Taarifa zinaeleza Cheka amepatikana na hatia ya kushambulia baada
ya kumpiga aliyekuwa Meneja wa baa yake.
Pamoja na
kifungo cha miaka mitatu, Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakamani hiyo, Said
Msuya amemhukumu Cheka kulipa faini ya Sh milioni moja baada ya kumaliza
kifungo hicho.
Cheka amepatikana na hatia ya shambulio dhidi ya aliyekuwa meneja wa baa yake,
Bahati Kibanda aliyemshambulia Julai 2, mwaka jana, katika Ukumbi wa Vijana
Social aliokuwa ameukodi kwa ajili ya kuendesha shughuli za baa zilizokuwa
zinasimamiwa na Kibanda.
Kutokana na kukutwa na hatia, Cheka amekuhukumiwa kwenda jela kwa muda huo na
imeelezwa tayari ameshapelekwa kwenye gereza mkoani humo.
|
No comments:
Post a Comment