MAFANIKIO SOKANI BAADA YA MIAKA 23:-Hizi ndio Picha za Mapokezi ya Mabingwa wa AFCON 2015 Ivory Coast walipowasili Nyumbani. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, February 11, 2015

MAFANIKIO SOKANI BAADA YA MIAKA 23:-Hizi ndio Picha za Mapokezi ya Mabingwa wa AFCON 2015 Ivory Coast walipowasili Nyumbani.

Yaya Toure na wenzake wakiwasili Ivory Coast baada ya kutwaa Ubingwa wa Kombe la Mataifa AFCON 2015 huko Estadio de Bata, Mjini Bata Nchini Equatorial Guinea Jumapili Februari 08,2015 dhidi ya Ghana.

Mabingwa wa kombe la Mataifa ya Africa, AFCON 2015 ni Ivory Coast, Dunia nzima ilishuhudia usiku wa Februari 08,2015,Jumapili huko Estadio de Bata, Mjini Bata Nchini Equatorial Guinea, Ivory Coast waliibuka Bingwa wa Mataifa ya Afrika kwenye Mechi ya Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2015,  walipoibwaga Ghana kwa Mikwaju ya Penati 9-8 kama walivyofanya Mwaka 1992.

Hii ni mara ya pili kwa Ivory Coast kutwaa Ubingwa wa Afrika na mara ya kwanza ni Mwaka 1992 walipoitoa Ghana pia kwa Mikwaju ya Penati 11-10 baada ya suluhu ya 0-0.

Hii pia ni mara ya pili kwa Kocha wa Ivory Coast, Herve Renard, kutwaa Ubingwa wa Afrika na mara ya kwanza ilikuwa 2012 alipoiwezesha Zambia kutwaa Ubingwa, tena kwa kuifunga Ivory Coast, na sasa kuweka Rekodi ya kuwa Mtu wa kwanza kutwaa Ubingwa wa Afrika na Nchi mbili tofauti.

Kwa Kocha wa Ghana, Avram Grant, hii ni mara ya pili kushindwa Fainali kubwa kwa Mikwaju ya Penati baada ya Mwaka 2008, akiwa na Chelsea, alipobwagwa kwa Mikwaju ya Penati na Manchester United kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI huko Moscow, Urusi.

Rais wa Ivory Coast, Alassane Ouattara aliongozana na maelfu ya mashabiki ambao walifurika kwenye mapokezi ya Mabingwa hao baada ya kuwasili nyumbani kwao.

Hapa ni baadhi ya PICHA za Mabingwa hao baada ya Kukabidhiwa kombe lao na wakati wakiwasili nyumbani kwao.
Rais wa Ivory Coast, Alasane Outtara na Yaya Toure katika mapokezi ya kikosi cha Timu hiyo ya Taifa.






Milango pekeyake haikutosha kuingilia Uwanja wa Felix Houphouet-Boigny, wengine walitumia njia hii.....UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad