![]() |
|
Simba SC wakimenyana na Mbeya City katika Uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam leo januari 28,2015 kwenye Mchezo wa Ligi kuu soka Vodacom Tanzania bara.
Simba SC
imeendelea kupoteza michezo yake hasa ya nyumbani baada ya leo Januari 28,2015 kukubali
tena kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City.
Mechi hiyo
ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) imepigwa muda mfupi uliopita katika Uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam na Mashabiki kushuhudia Simba SC wakikosa penati dakika za lala salama baada ya kugonga mwamba wa juu huku magoli ya mchezo huo yakifungwa kwa Simba SC na Ibrahim Salum Hajib na Mbeya City kwa Penati ya Yusuf Abdallah na Hamad Kibopile .
Simba SC hivi
karibuni ilipoteza mechi yake ya nyumbani baada ya kupigwa na Kagera Sugar
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaa, kabla ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya
Azam FC .
Matokeo hayo
ya kufungwa yanaiacha Simba SC ikiwa na alama 13 baada ya mechi 11 huku Mbeya
City ikifikisha alama 15 kwa mechi 11 pia.
UNGANANASI KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Wednesday, January 28, 2015
LIGI KUU VODACOM 2014/2015:-Januari 28,2015 Simba SC yachapwa na Mbeya City..
Tags
# MICHEZO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.






No comments:
Post a Comment