LA LIGA 2014/2015:-Real Madrid yauanza vibaya mwaka 2015 na Kufuta Rekodi ya Mechi 22 bila kufungwa January 4, 2015. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, January 05, 2015

LA LIGA 2014/2015:-Real Madrid yauanza vibaya mwaka 2015 na Kufuta Rekodi ya Mechi 22 bila kufungwa January 4, 2015.

Cristiano Ronaldo akiifungia Real Madrid bao la kuongoza kwa mkwaju wa penati leo January 04,2015 kwenye mechi ya Ligi kuu Hispania.

Mabingwa wa ulaya ,Real Madrid hii leo January 4, 2015,(jumapili) wameuanza vibaya mwaka 2015 baada ya kukubali kipigo cha 2-1 toka kwa Valencia katika mchezo wao wa 17 wa ligi kuu ya Hispania 2014/2015 na kufanya zile mbio za Mechi 22 za Real Madrid bila kufungwa katika Mechi rasmi za Mashindano.

Mchezo huo wa Ligi  uliopigwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Valencia Estadio Mestalla, Cristiano Ronaldo aliipa Real Bao la kuongoza wa Penati ya Dakika ya 14 lakini Valencia wakapiga Bao 2 Kipindi cha Pili kupitia Antonio Barragan na Nicolas Otamendi kuwapa Bao la ushindi.

Matokeo hayo yamewabakisha Real Pointi 1 mbele ya Barcelona ambao wanaweza kutwaa uongozi wakiifunga Real Sociedad baadae usiku wa leo January 4, 2015, ingawa Barcelona watakuwa wamecheza Mechi 1 zaidi.
Wachezaji wa Valencia wakishangilia bao la kwanza lililofungwa na Antonio Baraggan .

MATOKEO YA MECHI LA LIGA 2014/2015.

Jumamosi Januari 3,2015.

Atletico Madrid 3 – 1 Levante 

Sevilla 1 – 0 Celta Vigo 

Elche 2 – 2 Villareal 

Deportivo La Coruna 1 – 0 Athletic Bilbao 

Malaga CF 1 – 2 UD Almeria 

Jumapili Januari 4,2015.

Getafe CF 1 - 2 Rayo Vallecano

Valencia C.F 1 - 2 Real Madrid CF

2100 RCD Espanyol v SD Eibar

2300 Real Sociedad v FC Barcelona

Jumatatu Januari 5,2015.

2245 Cordoba CF v Granada CF

Wachezaji wa Real Madrid wakiwa wanatoka uwanjani kwa majonzi baada ya kufungwa na Valencia .
UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad