|
Akizungumza
katika Bunge hilo, Bw.Mbatia amesema kuwa kitendo cha Polisi cha kuwapiga raia
wasiokuwa na hatia, kuwazalilisha Waandishi wa Habari na kupiga mabomu ya
machozi kiasi cha kuwafanya watoto wadogo kuhangaika hakikubaliki.
Amesema Polisi
wakiendelea kuachwa kufanya vitu vya uvunjifu wa Amani, Serikali haitatawalika
hivyo ili kurejesha amani na imani ya wananchi kwa Serikali yao ni vema
shughuli zote za Bunge zikaahirishwa kupisha mjadala wa hoja hiyo binafsi kwa
lengo la kuinusuru nchi.
"Nimesikitishwa sana, Lipumba amepigwa, watoto wamepigwa, waandishi wa
habari wamepigwa, na Polisi wakasema wamepewa maagizo
"Prof Lipumba ni Mwenyekiti wa chama chenye wabunge zaidi ya 30 na
Mwenyekiti wa chama kinachoshiriki serikali ya Zanzibar, sasa kama yeye
anafanyiwa hivi itakuwaje Wananchi wa kawaida?
“Mheshimiwa
Spika naliomba bunge lako liahirishe shughuli zake ili leo tuweze kujadili
suala hili la uvunjifu wa amani uliofanywa na jeshi letu la polisi jijini
Dar es Salam jana, wao wanasema kuwa wamepewa amri kutoka ngazi za juu tunataka
serikali ituambie ni nani anayetoa amri hizi za kupiga watu wasiokuwa na hatia
yeyote, " amesema
Mbatia.
Baada ya
kuwasilisha hoja hiyo asilimia kubwa ya Wabunge walisimama juu ishara ya kuunga
mkono hoja hiyo lakini Spika wa Bunge,Bi.Anna Makinda akawaomba wakae ili aweze
kutoa ufafanuzi kwa mujibu wa kanuni.
Spika Makinda
aliwaeleza Wabunge hao kuwa suala hilo ni nyeti kwa sababu ni la kiusalama, ili
kupata ufafanuzi zaidi anaiagiza Serikali kufikisha Bungeni hapo majibu ya hoja
hiyo kesho Januari 29,2015 ili wabunge waweze kujadili.
Baada ya
maamuzi hayo ya Spika Makinda, kelele zikasikika Bungeni huku Wabunge wakitaka
kufanyika kwa mjadala huo leo leo, ndipo Spika alipoamua kuahirisha Bunge hadi
saa kumi jioni ambapo pia kutokana na hoja kutokamilika liliahirishwa mpaka
kesho Januari 29,2015 saa Tatu asubuhi.
Kiongozi
huyo wa upinzani inadaiwa alifika eneo ambako maandamano yaliyopangwa kufanyika
Jumanne Januari 27,2015,yalikuwa yamepigwa marufuku, ingawa uongozi wa chama
cha CUF unadai Profesa Lipumba alikusudia kuwashawishi wafuasi wake watawanyike
kutii amri ya polisi ndipo akashambuliwa.
Wakati huo
huo Profesa Lipumba amefikishwa mahakamani mjini Dar Es Salaam ambako amesomewa
mashtaka ya kufanya maandamano bila kuwa na kibali.
Hata hivyo
kwa muda Profesa Lipumba alikimbizwa hospitalini baada ya afya yake kudhoofika,
ikidaiwa ni sababu ya kupigwa na polisi.
Hata hivyo
alirejeshwa mahakamani baada ya kupata nafuu, na kesi yake imeahirishwa na
itatajwa tena mahakamani tarehe 26 Februari 2015.
Ameachiwa
kwa dhamana ya watu wawili kwa kiasi cha shilingi milioni mbili kila mmoja.
|
No comments:
Post a Comment