KOMBE LA MAPINDUZI 2015:-Simba SC yafuvu Robo Fainali kwa bao la Singano. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, January 06, 2015

KOMBE LA MAPINDUZI 2015:-Simba SC yafuvu Robo Fainali kwa bao la Singano.


Kikosi cha Simba sc kilichoanza Usiku wa jana January 05,2015.

 Wekendu wa Msimbazi Simba SC jana January 05,2015, imefuzu Robo Fainali ya Kombe la Mapinduzi 2015, kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi JKU katika mchezo wa Kundi C, uliofanyika Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Matokeo hayo yanaifanya Simba SC imalize kileleni mwa Kundi C kwa pointi zake Sita baada ya mechi tatu, mbele ya Mtibwa Sugar iliyomaliza na pointi tano.

 Simba SC katika mchezo huo walipata bao hilo, lililofungwa na Ramadhani Singano ‘Messi’ dakika ya 12 kwa shuti kali akiwa ndani ya boksi baada ya kupewa pasi nzuri na Said Ndemla.

Sifa zimuendee mshambuliaji Mganda, Dan Sserunkuma ambaye baada ya kupewa pasi na kiungo Jonas Mkude, aliwahadaa wachezaji wa JKU kabla ya kumpasia Ndemla aliyempa mfungaji.
 
Kikosi cha JKU kilichoanza jana .


 Baada ya mechi hiyo, kocha Kopunovic amesema timu yake inaimarika kidogo kidogo na ilicheza tofauti kwa vipindi vyote.

“Hii ni siku ya tano tu tangu nifike, bado naendelea kuwapa mbinu mpya. Wachezaji wangu kimbinu nawaona wazuri”-“Mimi napenda vijana ndio maana nawatumia wengi. Kidogo kidogo tutakuwa safi” Alisema Kopunovic.

Simba SC wanasubiri mpinzani wao wa Robo fainali katika mechi za Leo ambapo kutakuwa na mechi nne.

Majira ya saa 9:00 alasiri katika uwanja wa Amaan, KCC watachuana na KMKM, saa 11:00 jioni Azam FC watakabiliana na Mtende, hizo ni mechi za kundi B.

Kundi A, Taifa ya Jang’ombe itapepetana na Polisi katika uwanja wa Mao Dze Tung majira ya saa 9:00 alasiri.

Mtanange mwingine wa kundi A utawakutanisha Yanga SC dhidi ya Shaba majira ya saa 2:00 usiku uwanja wa Amaan.


 UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad