|
KUNDI A la
Mashindano ya Mataifa ya Afrika, AFCON 2015, Jana Januari 25,2015 Usiku lilicheza
Mechi zao za mwisho na Wenyeji Equatorial Guinea na Congo kufuzu kutinga Robo
Fainali baada za kuzitoa Gabon na Burkina Faso.
Gabon,
ikiongozwa na Nahodha Pierre-Emerick Aubameyang, Mchezaji wa Borussia Dortmund,
walichapwa Bao 2-0 na Equatorial Guinea Wenyeji wa Mashindano ya Kombe la
Mataifa ya Afrika, AFCON 2015, na kubwagwa nje wakati Wenyeji hao wakitinga
Robo Fainali kutoka Kundi A.
Kwenye
Dakika ya 55, Lloyd Palun wa Gabon alimwangusha Javier Balboa ndani ya Boksi na
Refa kuamua ni Penati iliyofungwa na Balboa mwenyewe.
Kinda
anaechezea Valencia huko Spain, Iban, aliwapa furaha kubwa Wenyeji Equatorial
Guinea kwa kuwafungia Bao la Pili katika Dakika ya 87 baada ya Javier Balboa
kumpasia Emilio Nsue ambae Shuti lake liliokolewa na kumfikia Iban aliemalizia.
Nao Congo wametinga Robo Fanali ya Kombe
la Mataifa ya Afrika kwa mara ya kwanza tangu 1992 bada ya kuichapa Burkina
Faso Bao 2-1 katika Mechi yao ya mwisho ya Kundi A la AFCON 2015 huko Mjini
Ebebiyin Nchini Equatorial Guinea.
Congo
walikwenda mbele Dakika ya 52 baada ya Ferebory Dore kumlisha Thievy Bifouma
ambae alifunga Bao kwa Congo na Burkina Faso kusawazisha Dakika ya 86 kupitia
Aristide Bance lakini Dakika 1 baadae Congo wakaenda Bao 2-1 mbele kwa Goli la
Fabrice Ondama baada Kipa Germain Sanou kuokoa Mpira kwa ngumi na kumgonga
Ondama Begani na kutinga.
RATIBA:**Saa
za Bongo
Jumatatu
Januari 26
KUNDI B
2100 Congo
DR v Tunisia [Estadio de Bata]
2100 Cape
Verde Islands v Zambia [Nuevo Estadio de
EbebiyÃn]
Jumanne
Januari 27
KUNDI C
2100 South
Africa v Ghana [Estadio de Mongomo]
2100 Senegal
v Algeria [Nuevo Estadio de Malabo]
Jumatano
Januari 28
KUNDI D
2100
Cameroon v Côte d'Ivoire [Nuevo Estadio de Malabo]
2100 Guinea
v Mali [Estadio de Mongomo]
|
No comments:
Post a Comment