Ofisi ya
Waziri Mkuu (TAMISEMI), imetangaza matokeo ya jumla ya Uchaguzi wa Serikali za
Mitaa uliofanyika Desemba 14 na 21,2014 yakionyesha kuwa uungwaji mkono wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM) katika maeneo ya mijini umeporomoka kwa kasi.
Katika
uchaguzi huo, chama kipya cha ACT-Tanzania kimechomoza na kuviacha baadhi ya
vyama vikongwe ambavyo havikupata hata nafasi ya ujumbe.
Akisoma
matokeo hayo jana,Desemba 24,2014 Mkurugenzi wa Uchaguzi wa TAMISEMI, Bw.
Khalist Luanda alisema matokeo hayo yamekamilika kwa asilimia 99 kutokana na
baadhi ya maeneo kutofanya uchaguzi kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo
wagombea kufungua kesi mahakamani na baadhi ya wagombea kufariki dunia kabla ya
uchaguzi.
Jumla ya
vyama 15 vilishiriki uchaguzi huo vikiwamo CCM, Chadema, CUF, NCCR - Mageuzi,
TLP, NLD, ACT, UDP na APPT- Maendeleo. Vingine ni Chauma, NRA, UMD na vitatu
ambavyo havikuambulia kiti hata kimoja vya DP, Tadea na ADC.
MATOKEO.
Pamoja na
CCM kuendelea kuongoza kwa ujumla, chama hicho kimeonekana kupoteza viti mijini
na vijijini na kimeporomoka zaidi mijini.
Katika
maeneo ya vijiji na vitongoji, chama hicho kimepata ushindi wa asilimia 79.81
(vijiji) na 79.83 katika vitongoji, wakati kwenye mitaa ambayo ipo sehemu za
mijini kimeshuka zaidi na kupata asilimia 66.66.
Matokeo hayo
yakilinganishwa na yale ya mwaka 1999, chama hicho kimepata asilimia 89.2
katika mitaa, asilimia 91 katika vitongoji na asilimia 91.6 katika vijiji.
MATOKEO
YA VIJIJINI.
Idadi ya
vijiji vyote Tanzania Bara vilivyotarajiwa kufanya uchaguzi ni 12,443 lakini
umefanyika katika vijiji 11,750.
Matokeo ya
vyama pamoja na asilimia katika mabano ni CCM 9,378 (79.8), Chadema 1,754
(14.9), CUF 516 (4.4), NCCR Mageuzi 67 (0.6) na TLP 10 (0.09).
Vingine ni
UDP 14, ACT 8 (0.07), NLD 2 (0.02), (0.12) na NRA 1 (0.0001).
UCHAGUZI
WA VITONGOJI.
Jumla ya
vitongoji vilivyotarajiwa ni 64,616 lakini vilivyopiga kura 60,688 huku CCM
ikiendelea kuongoza kwa kupata vitongoji 48,447 (79.8), Chadema 9,145 (15.1),
CUF 2,561(4.2), NCCR Mageuzi 339 (0. 6), ACT 72 (0.12, TLP 55 (0.1), UDP 54
(0.1), NLD 2 (0.02).
MATOKEO
YA MITAA.
Mitaa yote
3,875 nchini ilifanya uchaguzi na kukamilika kwa asilimia 100 huku CCM ikipata
asilimia 66.66 baada ya kupata mitaa 2,583, ikifuatiwa na Chadema iliyopata
mitaa 980 (25.3), CUF 266 (6.9), NCCR Mageuzi 28 (0.7), TLP 1 (0.03), ACT 12
(0.31), UDP 3 (0.08), NRA 1 (0.03) na UMD 1(0.03).
UKAWA
YACHANUA .
Kwa matokeo
hayo, inaonyesha kuwa vyama vinavyounda Ukawa vimeongeza nguvu katika maeneo
mengi hasa mijini ambako kwa pamoja vimepata wenyeviti 1,275 ikiwa ni sawa na
asilimia 32.18 ya mitaa yote.
Katika
maeneo ya vijiji Ukawa wamepata jumla ya vijiji 2,339 ambayo ni asilimia 19.91
wakati kwenye vitongoji waliambulia 12,047 sawa na asilimia 19.87.
WAJUMBE
VITI MAALUMU.
Kwa upande
wa wajumbe wa viti maalumu ambao safari hii wamepigiwa kura badala ya kutokana
na uwiano wa kura, CCM ilipata asilimia 80.24, Chadema (14.8), CUF asilimia
(4.31), NCCR asilimia (0.48), ACT (0.08) huku APPT Maendeleo, Chauma na NRA
vyote vikipata mjumbe mmoja kila kimoja sawa na asilimia 0.0001.
|
No comments:
Post a Comment