SAKATA LA ESCROW:- Ukawa walitaka Bunge kuiwajibisha Serikali. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, December 24, 2014

SAKATA LA ESCROW:- Ukawa walitaka Bunge kuiwajibisha Serikali.

Akizungumza jana Desemba 23,2014, Mwenyekiti wa Ukawa Profesa Ibrahim Lipumba akiwa na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na Katibu Mkuu wa Chadema, Wilbrod Slaa, alisema Kikwete anasita kumuondoa Muhongo wakati Bunge lililishatoa maazimio ya kutaka aondolewe.

 Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umelitaka Bunge kuiwajibisha serikali ikiwa Rais Jakaya Kikwete atashindwa kutekeleza maazimio ya Bunge ikiwemo kumng’oa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

Akizungumza Desemba 23,2014, Mwenyekiti wa Ukawa Profesa Ibrahim Lipumba akiwa na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na Katibu Mkuu wa Chadema, Wilbrod Slaa, alisema Kikwete anasita kumuondoa Muhongo wakati Bunge lililishatoa maazimio ya kutaka aondolewe.

Profesa Lipumba alisema Bunge linalowakilisha wananchi zaidi ya milioni 45 liliazimia uteuzi wa Muhongo utenguliwe lakini rais anasema bado anachunguza.

Profesa Lipumba alisema kama Rais Kikwete atashindwa kumwajibisha Muhongo atakuwa ameshindwa kutekeleza moja ya maazimio ya Bunge na kwamba Ukawa litaliomba Bunge kuiwajibisha serikali.

Alisema moja ya njia ya kuiwajibisha serikali ni pamoja na wabunge kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu.

Profesa Lipumba alisema “ hivi rais anachunguza nini haliamini bunge, kama anavyoteua mawaziri  pia ana madaraka ya kutengua nafasi zao, sasa anasita nini wakati ni azimio la bunge limemwelekeza, ikumbukwe kuwa bunge kwa niaba ya wananchi ndilo lenye jukumu la kuisimamia serikali,” - alisema Lipumba.

Alisema hotuba aliyoitoa Jumatatu wakati akiwahutubia wazee wa mkoa wa Dar es Salaam, haijakidhi matarajio ya wengi kwani kuna maazimio hayajatekelezwa.

Azimio ambalo halijatekelezwa na rais Kikwete ni lile linalotaka kutaifishwa kwa mitambo ya  IPTL na kutengua uteuzi wa Muhongo.

Mwenyekiti huyo alisema rais amekataa kutekeleza azimio la kutaka mitambo ya IPTL itaifishwe  na kutoa sababu ambazo hazina maana.

 “Tangu mitambo ya IPTL imefungwa taifa limepata hasara kubwa kwa sababu umeme unaouzwa na ni wa gharama kubwa kuliko mitambo yoyote ya umeme inayotumika katika bara la Afrika taifa limeingia hasara kubwa, rais aitaifishe,” alisema Profesa Lipumba.

Alisema katika hotuba hiyo rais alionyesha kuipendelea IPTL na kuikandamiza Tanesco wakati akielezea kuwa fedha za Escrow zilikuwa mali ya IPTL.

Hatua za kuchukua:-BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad