HII NI SEHEMU TU YA HOTUBA YA RAIS KIKWETE LEO DESEMBA 22,2014.
UCHAGUZI WA
SERIKALI ZA MITAA.
Anasema
zoezi lilikwenda ingawa kulikuwa na dosari kadhaa
Anapongeza
vyama vya siasa na wagombea na walioshinda,wafanye mikakati ya kuwaongoza
wananchi
Anamuunga
mkono Waziri Hawa Ghasia
kuwafukuza,kuwasimamisha kazi na kuwaonya waliovuruga uchaguzi,kwamba watumishi
wa Umma sharti wawajibishwe wanaposhindwa kusimamia majukumu yao.
Vurugu
wakati wa uchaguzi kuwa waliofanya vitendo vya uvunjaji wa sheria wakamatwe na
kuchukuliwa hatua
Kwamba
inawakatisha tamaa watu wema mhalifu akikamatwa na kuachiwa baada ya muda mfupi
bila hatua kuchukuliwa
KASHIFA YA
AKAUNTI YA ESCROW
Kwamba jambo
la pili linalofuata sio jema masikioni mwao
Anaanza
kueleza mwanzo wa sakata lilivyoibuka Bungeni
Kwamba
Serikali ilihaidi na kumtaka Mkaguzi wa Serikali kukagua,na kuiagiza TAKUKURU
kuchunguza mwenendo wa miamala na hatua
zichukuliwe kwa mujibu wa mamlaka waliyonayo na kuwa yoote mawili yaliyohaidiwa
na Serikali yalifanyika na taarifa ya CAG iliwasilishwa Bungeni,kuwa ni zama za
ukweli na uwazi aliagiza pia taarifa ichapishwe kwenye vyombo vya habari ili
wananchi waifahamau.
Tarehe
8/Des/2014 baadaya ya kurudi nchini alisema ya Dodoma atayafahamu baadaye
kwamba baadhi ya magazeti yalimkariri akisema akwepa ESCROW kiaina.
Baada ya
kuletewa taarifa alianzakuisoma na kutoa maagizo ya ufuatiliaji ili kujua
ukweli na kuwa baadhi zinaendelea kufanyiwa kazi kupata ukweli na ameamua
kuzungumza ili kupunguza joto lililopo kuhusu sakata hilo
Kwamba kuna
mambo manne muhimu
AKAUNT
MMILIKI
KODI ZA
SERIKALI
TUHUMA ZA
RUSHWA
1.AKAUNTI YA
ESCROW
kwamba kuna mkataba wa tozo la umeme'capital
charge' na
2.Tozo ya
uwekezaji'Capacity charges'
Katika
mikataba hiyo yapo makubaliano kama utatokea mzozo,upo utaratibu uliowekwa
kushughulikia tofauti inayohusu migogoro ya kiuwekezaji
1998 Tanesco
na IPTL walifikishana mahakamani Tanesco ikilalamika kuwa kwenye tozo IPTL
inawatoza gharama kubwa kuliko uwekezaji waliofanya mashauri endelea mpaka
2001.Katika uamuzi mahakama ilikubali malalamiko ya Tanesco na ikafanya uamuzi
wa kupunguza tozo ya uwekezaji iliyotozwa na IPTL
Baadaye
tanesco wakaanza vurugu kuwa wanaweza kupata punguzo zaidi,kuwa katika
ukokotoaji wa kiwango cha tozo sio sawa na kuamua kutafuta nafuuu zaidi na
kukubaliana maadamu kuna mzozo,tuanishe akaunti ya ESCROW na ifunguliwe Benki
Kuu na wakaingia Mkataba Wizara kwa Niaba ya Tanesco na IPTL na Benki Kuu kama
wakala katika Mkataba huo.
Masharti ya
Akaunti kuwa bado kampuni ya IPTL itaendelea kupeleka madai yake Tanesco ya
Tozo na Tanesco itaendelea kulipa madai wanayopelekewa,na malipo hayo yapelekwe
ESCROW Akaunti mpaka tofauti zitakapoisha na fedha kutolewa kwa
muhusika.5/JULAI/2006 Akaunti ilifunguliwa
Kwamba
mgogoro umekaa miaka saba bila kupata suluhisho
na katika kipindi hicho Tanesco iliendelea kulipa
Kwa mujibu
wa TAARIFA YA CAG tarehe 20/Novemba/2014 akaunti ilikuwa na zaidi ya Bilioni
nane kwamba kwa fedha ya Tz ilikuwa nu
202.9 bilioni
Kwa mujibu
wa mkataba wa kununua umeme Tnesco isipolipa inatozwa riba ya asilimia mbili na
ilikuwa inadaiwa na IPTL
Kwamba kwa
mujibu wa taarifa alizopata na maelezo aliyotoa inasaidia kuweka kumbukumbu
sahihi anasisitiza hadi taarifa ya CAG inatolewa zilikuwa 202bilioni ndizo zilikuwa katika akaunti na sio306
bilioni kama zinazvyoelezwa na watu wengine
Kwamba ni
matumaini yake maelezo hayo yanasaidia kupata jibu la swali maarufu kuwa fedha
za nani za Umma au IPTL
AKAUNTI YA
ESCROW NI NINI?
Kwamba ni
tofauti na akaunti nyingine zote ambayo ni maalumu inayonzishwa kwa sababu
maalumu,kufanya kazi maalumu,mashart maalumu na kazi ikiisha akaunti hiyo
hufungwa
Kwamna
husimamiwa na wakala aliyekubaliwa na pande zote,ndiye mwenye jukumu la
kuisimamia na kumlipa mwenye fedha wakati ukifika
Kuwa Akaunti
ilianzishwa na Tanesco na IPTL na Benki ku ikawa Wakala na kutoa nafasi ya
pande husika kushughulikia tofauti zao
Kimsingi
fedha ni mali ya IPTL kwani ndiye mlipwaji kwa kuidai Tanesco kuhusu tozo la
uwekezaji
Katika swali
la fedha za umma,mdhibiti alipulizwa alisema inawezekana zipo na Umma na IPTL
Mkaguzi
Aliposema inawezekanakuna fedha za umma maanayake kama mgogoro ungetatuliwa na
kama madai ya Tanesco yangekubaliwa kuna fedha ya Tanesco ambayo
wangerudishiwa na kuwa bahati mabay
miaka saba halikufanyika na baadaye kutekelezwa uamuzi wa kufungwa akaunti na
IPTL ipewe fedha yake.
Maana
nyingne kwamba kuna kodi ya Serikali,Taarifa ya CAG kwamba kulikuwa na kodi
ambayo haikulipwa,ambazo ni bilioni 21.7 ,Kuwa TRA ilipeleka madai yake kwa PAP
kutaka ilipwe na kuwa hakuna haki ya fedha ya Tanesco
Katika
ukaguzi wa hesabu za Tanesco mwaka 2012 CAG
aliwaelekeza kuacha kuhesabu fedha za akaunti ya Escrow kama fedha
yao,kuwa hata kama mwenyewe alikuwa ajazichukua hizo hazikuwa zao na kuwa fedha
hizo hazikuwa na sifa ya kutafsiliwa kama fedha za Tanesco
Kwamba 5/Des/2013 Mahakama ilitoa uamuzi wa suala hilo
Kwamba
Mjadala kuhusu Escrow uliibuka Serikalini
kuhusu fedha zilizopo kuhusu fedha zitoke au zibaki,Nishati
walimwandikia Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye alishauri kutekelezwa kwa
uamuzi wa Mahakama kuu
Kwamba Benki
kuu nao walifuata ushauri wa Mwanasheria Mkuu ambaye alisema pia hakuna kodi ya
kulipwa na kwa kuzingatia ushauri huo Akaunti ilifungwa na fedha kupewa IPTL
KUWA BAADA
YA HAPO MJADALA ULIHAMIA KWENYE BUNGE NA MITANDAO YA kIJAMII kuwa imeibuka
kashifa kubwa kuhus fedha hiyo
Uamuzi ule
ulitiliwa shaka kuwa haukuwa sahihi na kuonekana umeitia nchi hasara na kuibua
hisia kwamba sio bure kuna namna ya kuwepo mazingira ya rushwa na watu
kunufaika binafsi kila mmoja akisema mambo yake,kila na kurushiana lawama za
fulani kala fedha,kuwa fedha zimebebwa kwenye viroba,sandarusi,rumbesa lakini
jambo moja
Alipokutana
na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupata maoni yake alisema hakukosea katika ushauri wake na uamuzi wa mahakama ilikuwa sahihi
Kwamba
hakuna hasara iliyokuwa imepatikana kwa kuwa ililipwa kwa mtu sahihi na kuwa
Akaunti hiyo ilianzishwa kutunza fedha za tozo za uwekezaji kwa IPTL
Kuwa KUWEPO
KWA aKAUNTI YA ESCROW hakubadili kuwepo kwa mwenye fedha zake ambaye ni
IPTL anasisitiza Taifa halikupata hasara
Kuwa
Mwanasheria alimwambia hakuna Kodi ya Serikali na kama mamlaka husika inaona
kuna kodi ya kulipwa waendelee kufuatilia
Anasema hili
sakata lina vurugu nyingi.
Anasema kuwa
hata Umiliki wa kampuni wa PAP ulianza kutiliwa shaka
Anafafanua
kuhusu makampuni yanayohusika katika sakata hili na uhalali wa kuuziana hisa na
kuwa haikuwa lazima mamlaka nyingine za Serikali kufahamu
TUHUMA ZA
RUSHWA KATIKA MCHAKATO
Kuwa
wamesikia mengi na yataendelea kuwepo na yameandikwa mengi na mengine bado
hawjayasoma kuwa rushwa ni tendo la jinai na kuwa taarifa za haruz ya rushwa
aliagiza zipelekwe TAKUKURU,kuwa kuna yaliyobainika na kupewa taarifa ya awali
na kuagiza yafanyiwe uchunguzi zaidi
Kwamba
miamala kwenye Akaunti ya Escrow kwenye Benki ya Mkombozi kuwa Serikali
inahusika na Watumishi wa Umma,na hivyo uchunguzi hautawahusu Rugemalila na
watu wengine walioko nje ya Utumishi wa Umma,kuwa TAKUKURU na Tume ya Maadili
itawahoji watuhumiwa
Kwamba hata
waliokutwa na mamilioni kwenye akaunti zao nao watahojiwa na vyombo husika
MAAZIMIO YA
BUNGE
Kuwa
Serikali imeyapokea na watayafanyia kazi na wameanza kufanya hivyo na
kuwapongeza Wabunge kwa moyo wa kuchukia maovu na kuwa yuko pamoja na Wabunge
katika mapambano hayo
Kwamba
haikuwa kazi rahisi kuwa ilikuwa kazi pevu,kuwa wamefanya kazi nzuri na mambo
yameisha salama na kuwa kuna maazimio yanayozungumzika na yanayotekelezeka
Anashukuru wajumbe wa Tume ya Bunge Zito Kabwe,Filikunjombe na wengine
Mwisho
anapongeza michango ya wabunge na ushirikiano wa Wabunge wa CCM na Upinzani na
kuwa inatakiwa kuwa hivyo katika mazingira kama hayo.
Kwamba
alivyosikia upinzani wakitaka kufanya uamuzi wa Bunge kama ajenda yao binafsi
na kuwa sio kweli CCM imafumbia macho wala rushwa na kuwa hata magerezani kuna
wafungwa kutoka pande zote za vyama,ningeshangaa mbunge wa CCM kupinga jambo
hili eti kwa ababu ya mapenzi na chama chake.
Kamati ya
Bunge ilikuwa na Wabunge wa CCM wengi na kuwa kama wangeweza kukataa hoja
ziziwasilishwe wangeweza kufanya hivyo kuwa sio kweli kuwa ccm haichukii rushwa
Kwamba
walisema kwa uchungu juu ya uovu huo ila wapinzani wanatumia ajenda hiyo kupata
sifa kwa urahisi.
Kwamba
waliofanya vitendo viovu sio wenzao na CCM,kuwa bado Serikali ina dhamira ya
kweli kuipinga rushwa.
1.Pendekezo
la Kuchukua Mitambo ya IPTL wamelijadili na katika kipindi hiki utekelezaji
wake hauwezekani hasa kulingana na ugumu wa mazingira ya utaifishaji,kuwa
wawekezaji watakimbia,kwambamatatizo ya IPTL yashughulikiwe vizuri bila kujenga
taswira mbaya.
2.Uwazi wa
Mikataba-Hilo litafanyika na kuwa moja linahitaji muda zaidi ya kulipitia kwa
kuwa kuna kanuni za usiri katika biashara ili kujiridhisha na utunzaji wa siri
kama mikataba inavyotaka,kuna mambo wanaweza kukubaliana ili kulitekeleza.
3.Takukuru,Polisi
wachukue hatua kwa waliotajwa kwenye Tarifa ya Kamati-Kuwa hatua zinaendelea
4.Kuwavua
wadhifa Wenyeviti wa Kmati za Bunge waliotuhumiwa-Ni jukumu la Bunnge lenyewe
5.Rais
kuunda Tume ya Kijaji kuchunguza majaji waliotajwa katika kashifa-Amelipokea na
kulijadili kuwa namna ya utekelezaji itabidi lizingatie utaratibu wa Kikatiba
na Kisheria jinsi ya kushughulikia suala hilo na kuwa sharti lianzie kwenye
mahakama na sio kwa Rais.Ameachiwa Jaji Mkuu suala la Majaji
6.Kwamba
Mamlaka husikika za Kifedha na Kiuchunguzi ziitaje Stanibic kujihusisha na
utakatishaji wa fedha zitangazwe kama taasisi zinazotiliwa shaka-Ni pendekezo
zuri kuna kitengo maalumu kilichopewa jukumu la kuchunguza ili utaratibu wa
sheria uzingatiwe
7.Serikali
iwasilishe mswada wa Sheria,ili Takukuru iweze kupambana na Rushwa kubwa-Kuwa
mchakato wa kufanya mageuzi ndani ya Takukuru ulianza zamani na unaendelea na
kuwa ni jukumu la Takukuru kupeleka mapendekezo ya mambo wanayoona yanatakiwa
kufanyiwa mapendekezo.
8.Waziri wa Nishati na Madini,Waziri wa Ardhi,Bodi
ya Wakurugenzi Tanesco,Katibu Mkuu Nishati wawajibishwe-Kuwa Bodi ya Tanesco
imemaliza muda wake tumeanza mchakato hilo suala limejifuta lenyewe siku tano
zijazo bodi,Katibu Mkuu wa Wizara tumejadili ni Mtumishi wa Umma tuhuma zake
zichunguzwe kwanza ili atendewe haki,Mwanasheria ameishajiuzulu,Waziri wa Ardhi
kupokea fedha kutoka VIP tumekaa na kuzungumza,Kamti ya maadili wanaendelea
kuchunguza tuhuma zake,ulizwa fedha za nini amezipata kwa ajili gani,Bodi
imeeleza kuwa kwa nini fedha hazikwenda kwenye shule zikaenda kwenye Akaunti
yake,kuwa ni Masharti aliyopewa na mtoa fedha,kwa hiyo tumelitafakali sana kuna
msingi mkubwa wa kimaadili kuna upugufu tumemuomba ajiuzulu atupe nafasi
tumteue mwingine.
Waziri wa Nishati na Madini huyu tunamweka kiporo
kuna uchunguzi ameagiza ufanywe hajapata majibu na baada ya uchunguzi uamuzi
utafanywa kwa misingi ya Haki.
Huo ndi
mwanzo na Mwisho wa Hotuba yangu ndefu,Asanteni sana
UNGANANASI
KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
No comments:
Post a Comment