MATOKEO YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA 2014:-CCM ‘yapoteza’ viti 2,600 Serikali za Mitaa . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, December 18, 2014

MATOKEO YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA 2014:-CCM ‘yapoteza’ viti 2,600 Serikali za Mitaa .

Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imetangaza matokeo ya awali ya uchaguzi wa Serikali za mitaa Uliofanyika Desemba 14,2014,nchi nzima yanayoonyesha kuimarika kwa upinzani.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Bw. Khalist Luanda alisema jana Desemba 17,2014,kwamba wakati Chama cha Mapinduzi - CCM ikifanikiwa kupata ushindi wa jumla wa mitaa na vijiji 9,406, kwa pamoja vyama vingine vya upinzani, vimegawana nafasi 3,211.

Kwa ushindi huo ,upinzani umeongeza viti 1,981 ikilinganishwa na uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliopita mwaka 2009 ambao kwa ujumla, ulipata nafasi 1,230 za wenyeviti wa mitaa na vijiji.

Kwa upande wake, CCM imepoteza nafasi 2,636 za uenyekiti wa vijiji na mitaa ikilinganishwa na uchaguzi wa mwaka 2009 ilipopata jumla ya viti 12,042.

Hata hivyo, uchaguzi mwa mwaka huu (2014), umefanyika huku kukiwa na nyongeza ya mikoa, wilaya, mitaa na vijiji katika baadhi ya maeneo nchini.

 Akitangaza matokeo hayo, Bw.Luanda alisema katika nafasi ya vijiji ambavyo matokeo yake yamepokelewa ni jumla ya vijiji 9,047 ambapo CCM ilipata 7,290 sawa na asilimia 80.58, Chadema 1,248 sawa na asilimia 13.79 na TLP viwili sawa na asilimia 0.02.

Vyama vingine ni CUF vijiji 382 sawa na asilimia 4.22, NCCR-Mageuzi 14 sawa na asilimia 0.15, NLD viwili sawa na asilimia 0.02 na ACT vinne sawa na asilimia 0.04.

Kwa upande wa mitaa 3,231,  CCM ilipata 2,194 sawa na asilimia 67.90, Chadema 828 sawa na asilimia 25.63, CUF 235 sawa na asilimia 7.27,  NCCR Mageuzi minane sawa na asilimia 0.25, TLP mmoja sawa na asilimia 0.03, NLD tisa sawa na asilimia 0.28, UDP mmoja sawa na asilimia 0.03  na ACT mmoja sawa na asilimia 0.03.

Akizungumzia upande wa vitongoji 42,824, alisema CCM ilipata 35,564 sawa na asilimia 83.05, Chadema 5,970 sawa na asilimia 13.94, CUF 1,555 sawa na asilimia 3.63, NCCR-Mageuzi 80 sawa na asilimia 0.19, TLP 11 sawa na asilimia 0.03, NLD kimoja sawa na asilimia 0.00, ACT 10 sawa na asilimia 0.02 na UDP 21 sawa na asilimia 0.05.

Matokeo hayo yamejumuisha maeneo mengi ambayo CCM ilipita bila ya kupingwa.

Katika matokeo hayo, CCM imeendelea kufanya vizuri katika mikoa ambayo imekuwa ikitajwa kuwa ni ngome yake lakini kuna maeneo ambayo yalionekana kuyumba kwa kuzolewa na upinzani.

Mfano wa ngome ambazo CCM kimetikiswa zaidi ni Mkoa wa Dodoma katika wilaya za Kondoa na Chemba ambako vyama vya CUF na Chadema vimefanya vizuri tofauti na uchaguzi uliopita.

Kuhusu nafasi ya mwenyekiti ambaye alisimikwa na wananchi kibabe katika Mkoa wa Arusha, Luanda alisema TAMISEMI haitamtambua, bali atakuwa ni mwenyekiti wa kimila tu.

UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad