|
Siku chache
baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Hawa Ghasia kuahidi
kumuwajibisha yoyote aliyehusika na kuvuruga uchaguzi wa Serikali za mitaa
uliofanyika tarehe 14, leo Desemba 17,2014,Waziri huyo ametangaza majina ya Wakurugenzi watano
waliosimamishwa kazi na wengine sita waliopewa onyo kutokana na uchunguzi
kuonyesha wameshindwa kutekeleza wajibu wao.
Majina ya
Wakurugenzi waliotajwa kusimamishwa ni haya; Felix Mabula (Halmashauri
ya Hanang), Fortunatus Fwema (Halmashauri ya Mbulu), Isabella
Chilumba (Halmashauri ya Ulanga), Pendo Malabeja (Halmashauri
ya Kwimba) na William Shimwela (Halmashauri ya Sumbawanga).
“…Ni
dhahiri kuwa Wakurugenzi wa kwenye zile Halmashauri zenye dosari wameonyesha
udhaifu mkubwa sana wa kutekeleza majukumu yao ikiwemo jukumu la msingi la
kusimamia uchaguzi ambao ni moja ya majukumu ya Wakurugenzi. Kasoro hizo
zilisababisha kurudiwa kwa uchaguzi katika baadhi ya maeneo yao… Wakurugenzi
hao wametenda makosa yafuatayo ambayo yanawaondolea sifa ya kuwa wakurugenzi
katika halmashauri…“– Hawa Ghasia.
“… Kwanza
ni kuchelewa kuandaa vifaa vya kupigia kura, kukosa umakini katika kuandaa
vifaa vya kupigia kura na hivyo kuchanganya majina pamoja na vyama, kuchelewa
kupeleka vifaa kwenye maeneo ya kupigia kura, uzembe katika kutekeleza majukumu
yao na kutoa taarifa za kupotosha kuhusu maandalizi ya uchaguzi.. kwa sababu
walituhakikishia kwamba maandalizi yamekamilika huku wakifahamu kwamba suala
hilo sio kweli…“– Hawa Ghasia.
|
No comments:
Post a Comment