![]() |
Kipa Peter Manyika alifanya kazi nzuri dakika ya 44, baada ya kuokoa mkwaju wa
penalti wa beki David Luhende. Penalti hiyo ilitolewa na refa Amon Paul wa Mara
baada ya kiungo Awadh Juma kumchezea rafu kwenye eneo la hatari mshambuliaji
Ame Ally.
Kipindi cha pili, Mtibwa Sugar walicharuka na kuanza kupeleka mashambulizi ya nguvu
zaidi langoni mwa Simba SC,Hali hiyo iliwafanya vinara wa hao wa Ligi Kuu
wapate bao la kusawazisha dakika ya 58, mfungaji Mussa Hassan Mgosi aliyetumia
makosa ya beki wa kulia, William Lucian ‘Gallas’ kuchanganyana na kipa wake,
Manyika Jr.
|
Nalo ba
pekee la kiungo Paul Ngway, dakika ya 52 jioni ya leo November 01,2014, limeipa Kagera Sugar
ushindi wa 1-0 dhidi ya Yanga SC, Uwanja wa Kaitaba, Bukoba katika mchezo wa
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Yanga SC ilimaliza mchezo huo pungufu, baada ya Nahodha wake, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 80 na refa Abdallah Kambuzi wa Shinyanga, baada ya kumpiga kichwa Rashid Mandawa wa Kagera. |
Ngway, mchezaji mkongwe wa timu hiyo ya Wakata Miwa wa Misenyi, Bukoba Vijijini,
alifunga bao zuri kwa shuti kali akimalizia krosi ya Julius Kwangwa.
Yanga SC
inabaki na pointi zake 10 baada ya mechi sita, ikishinda tatu, sare moja na
kufungwa mbili, nyingine na Mtibwa Sugar mjini Morogoro 2-0.
|
Nalo goli
pekee la Jacob Massawe dakika ya 15 limeipa ushindi wa 1-0 Ndanda FC dhidi ya
mabingwa watetezi, Azam FC Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara katika mchezo wa
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Huo unakuwa mchezo wa pili mfululizo, Azam FC kupoteza baada ya Jumamosi iliyopita kuchapwa 1-0 pia na JKT Ruvu Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Matokeo hayo, yanaifanya timu hiyo ya Alhaj Sheikh Said Awadh Bakhresa na familia yake ibaki na pointi zake 10, baada ya mechi sita, wakati Ndanda saa inadikisha pointi sita.
Mechi nyingine za ligi hiyo leo November 01,2014, Coastal Union imeilaza 1-0 Ruvu Shooting Uwanja wa Mkwakwani, Tanga bao pekee la Itubu Imbem dakika ya 54, wakati JKT Ruvu imefungwa 2-1 na Polisi Moro Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Karibu
kwenye familia ya Makonda Blog na uzipokee Picha/Habari zote kwa kutumiwa Mchana
/Usiku baada tu ya kujiunga kwa kubonyeza hapa mtu wangu >>>BONYEZA HAPA.>>>Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
No comments:
Post a Comment