AJALI:-Picha wakati Moto ulizuka kwenye Jengo la wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga Complex) Jijini Dar es Salaam . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, November 14, 2014

AJALI:-Picha wakati Moto ulizuka kwenye Jengo la wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga Complex) Jijini Dar es Salaam .


Moshi ukiwa umetanda angani Wakati Moto mkubwa uliozuka leo November 14,2014, mchana katika jengo la biashara Machinga Complex Ilala jijini Dar es salaam, umedhibitiwa baada ya kutekeza mali katika baadhi ya maduka.

Mwenyekiti wa bodi ya usimamizi wa jengo la Machinga Complex, Godwin Mmbaya amesema moto huo umedhibitiwa na hali ni shwari.
Tunashukuru Mungu moto umedhibitiwa kabla haujasambaa zaidi, kikosi cha zimamoto kiliwahi mapema na kilisaidia kufanikisha kuzima moto. Hakuna mtu alieyeumia zaidi ya kuteketea kwa mali kwenye maduka ambayo moto ulitokea, bado hatuna tathimini ya mali zilizoteketea, chanzo cha moto ni fundi alikuwa anakata kitu na mashine sasa vile cheche zikadondokea kwenye kitu, moto ukatokea na kuchanganya, sisi kwanza tunawapa pole wale wote waliopotelewa na mali zao kwa moto,” alisema Godwin.

Katika hatua nyingine Godwin alisema material yaliyotumika kujengea jengo hilo ni material ambayo hayawezi ungua na moto hali iliyosaidia moto huo kutosambaa mbali zaidi
Karibu kwenye familia ya Makonda Blog na uzipokee Picha/Habari zote kwa kutumiwa Mchana /Usiku baada tu ya kujiunga kwa kubonyeza hapa mtu wangu >>>BONYEZA HAPA.>>>Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp

Make Money at : http://bit.ly/adflywin

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad