AFYA YETU:-Watoto wanaoishi Mikoa ya chakula kingi ‘wanapoongoza’ kwa utapiamlo..' - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, November 04, 2014

AFYA YETU:-Watoto wanaoishi Mikoa ya chakula kingi ‘wanapoongoza’ kwa utapiamlo..'


UTAPIAMLO unaosababishwa na ukosefu wa lishe bora na matunzo sahihi unaendelea kuwa sababu ya watoto kudumaa na kutishia maisha yao.
Wakati nchi yetu kupitia mikakati mbalimbali ikiendelea kupambana na tatizo hilo, Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) linabainisha kuwa tayari nchi 63 duniani zinazoendelea zimefikia malengo ya Milenia katika vita dhidi ya utapiamlo mkali ifikapo mwaka 2015.

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza, anatahadharisha kuwa ni jambo la fedheha kubwa kwa nchi yetu kuendelea kukabiliwa na tatizo la udumavu unaosababishwa na ukosefu wa lishe bora na matunzo sahihi wakati kimsingi hatuna tatizo kubwa la chakula.

Kadhalika anasema ni jambo lisilovumilika kuendelea kupoteza maisha ya watoto 130 kila siku nchini kutokana na kukosa lishe bora. 

Anasema lishe duni inaathiri kwa kiasi kikubwa ukuaji wa kiakili wa watoto na hivyo kupunguza uwezo wa kufanya vizuri shuleni, hali ambayo pia inapunguza ufanisi katika maisha ya utu uzima wake.

Waziri Chiza anayasema haya katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dk Rajab Rutengwe, katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Chakula Duniani yaliyofanyika kitaifa Oktoba 16 mwaka huu katika Mji wa Mpanda.

Anakumbusha kuwa wakati tunapoadhimisha Siku ya Chakula Duniani, hatuna budi kujikumbusha kuwa madhara makubwa yanaweza kutokea katika ukuaji wa kimwili na kiakili kwa mtoto ikiwa lishe bora haitazingatiwa.

Kwamba tangu mimba inapotungwa mjamzito anatakiwa apate lishe bora na baadaye mama na mwanawe waendelee kupata lishe bora hadi mtoto anapotomiza angalau umri wa miaka miwili.

Hivyo ni jambo la msingi kwetu sote tukaelewa kuwa tunapoongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara, hatuna budi kuweka mkazo mkubwa katika kuboresha lishe ya familia zetu. Itakuwa haiingii akilini iwapo ongezeko la uzalishaji haliwezi kwenda sambamba na upunguzaji wa tatizo la utapiamlo na kudumaa kwa watoto,” anasisitiza.

Karibu kwenye familia ya Makonda Blog na uzipokee Picha/Habari zote kwa kutumiwa Mchana /Usiku baada tu ya kujiunga kwa kubonyeza hapa mtu wangu >>>BONYEZA HAPA.>>>Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

Copy n Win at: http://bit.ly/copyandwin

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad