Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu
Issa Machibya akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kituo cha redio jamii
Uvinza FM chini ya ufadhili wa Shirika la UNESCO na kampuni ya simu za mkononi
ya Airtel Tanzania.
Wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kulia ni Meneja wa huduma
za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi, Mwalikishi wa Shirika la Kimataifa
la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambaye pia ni mshauri na mkufunzi wa
redio jamii Bi Rose Haji Mwalimu pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Uvinza FM
Radio Bi. Nuru Kalufya.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu
Issa Machibya amesisitiza uadilifu katika vyombo vya habari jamii kwa kutangaza
habari zisizoumiza hisia kwa wananchi wengine na kuepuka migogoro.
Akizindua kituo cha redio jamii cha Uvinza FM,
Septemba 30,2014,Luteni Kanali Mstaafu Machibya alisema kuwa vyombo vina wakati
mgumu hasa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2015.
“Changamoto hii inaweza kuepukika kwa
kuhakikisha habari zinazotolewa zinalenga kuendeleza utamaduni wa amani,
upendo, utulivu na uvumilivu na kuepuka viashiria vinavyoweza kusambaza chuki
kwa lengo la kufanikisha chaguzi salama.
Mkuu wa Mkoa huyo amesisitiza umuhimu wa kuutumia
uhuru wa kutoa na kupata habari vizuri kwa kusema kwamba uhuru huo usitumike
kutoa habari zinazopendelea upande mmoja na kukandamiza mwingine kwa kuwa hali
kama hiyo husababisha machafuko.
“Kwa mujibu wa Ibara ya 18 (b) ya Katiba ya
Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, kila mtu anayo haki ya kutafuta,
kupokea na kutoa habari bila ya kujali mipaka ya nchi, lakini haki hiyo iende
sambamba kwa kuzingatia Sheria za nchi na kuhakikisha habari hizo haziumizi
hisia za wananchi wengine,”
|
No comments:
Post a Comment