Kwa hali ya
kushangaza, kituo cha television cha matangazo cha tbc 1 kati ya vituo vinne
maarufu vya matangazo ya habari nchini Tanzania kimeshika nafasi ya mwisho
baada ya kufanyiwa utafiti.
Kwa habari
za uhakika ni kwamba kituo kilichoongoza kuangaliwa na watazamaji wengi ni ITV
kikifuatiwa na Star TV, nafasi ya tatu imeshikwa na Channel 10 na hatimaye
TBC1.
Kwa utafiti
uliofanya na na TCRA imebainika kuwa ni aibu kama kituo television ambacho ni
cha Taifa na ni UMMA kushika mkia nyuma ya vituo binafsi jambo ambalo ni
hatari.
Vyanzo vya
kuaminika vinadai kuwa TBC1 imefikia hapo baada ya kugundulika inabagua baadhi
ya habari ya vyama vya siasa na kutoa habari ya chama kimoja tuu jambo ambalo
siyo sahihi katika utashi wa utangazaji na kutofuata uhuru wa kiutangazaji
ndani ya uongozi wa shirika la habari la Tanzania.
Utafiti
umeonyesha kuwa ili chombo cha habri kiweze kuangaliwa na watu wote wa vyama
vyote ni lazima chombo cha habari kitoe habari bila kubagua vyama vya siasa
maana watazamaji wana misimamo tofauti na itikadi tofauti, na kama chombo cha
habari kikiamua kutoa habari kwa chama kimoja cha siasa basi ujue hapo
watakaoangali hizo taarifa za habari ni hao hao wa chama kimoja.
Watafiti pia
walienda mbali zaidi na kukinyoshea vidole kituo cha taifa cha utangazaji kuwa
ni chombo cha UMMA na kisipende kubagua baadhi ya taarifa za habari za vyama
vya siasa kwa misingi ya kuelekezwa na wanasiasa au viongozi wa nchi maana
madhara yake ni wananchi kushindwa kuangalia hicho kituo.
Mwisho wake
kitashindwa kufanya biashara na hatimaye kutegemea tuu ruzuku serikalini na hapo
ndo nchi itazidi kupata hasara badala ya kukiacha chombo kijiendeshe kwa
uhuru.
Wametoa
mfano kama shirika la habari la Uingereza BBC lingefanya kama TBC inavyofanya
basi nayo ingeishia kutazamwa tuu nchini uingereza na tena kwa watu wachache
tofauti na ilivyo sasa BBC inatazamwa duniani kote.
Utafiti
umeonyesha kuwa hivi vyombo vingine vya habari ITV, Star TV na Channel 10
vimepata watazamaji wengi kwa kuwa havibagui matangazo ya kada tofauti ya vyama
vya siasa na hapo ndoo inasababisha waweze kupata watazamaji wa kutosha.
Chanzo:-Lukanza Blog.
|
No comments:
Post a Comment