Katika hali
isiyokuwa ya kawaida bibi mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa Miaka (65) ambaye
hakujulikana jina lake wala makazi yake amenusurika kuuawa na wananchi baada ya
kudhaniwa kuwa ni mchawi.
Tukio hilo
lililoshangaza na kushtua wakazi wa wilaya ya Geita mkoani Geita limetokea jana
Septemba 02,2014,majira ya saa 3.30 asubuhi katika mtaa wa Tambuka reli ikiwa ni kilomita chache
tu kufika Stendi ya Magari madogo yanayokwenda katika vijiji vya mkoa huo.
Akizungumzia
tukio hilo mmoja wa mashuhuda, Joyce Mcherwa ambaye ni mfanyabiashara wa eneo
hilo alisema yeye alikuwa anafagia nje ya kibanda chake na kushangaa mama huyo
anaanguka kutoka angani bila kuwa na kitu chochote.
Alisema mama
huyo alikuwa uchi wa mnyama amejifunga kitambaa chekundu kichwani na hirizi
shingoni.
Joyce
aliongeza kuwa mama huyo alikuwa hajitambui huku akihangaika kupaa tena
kwa kurusha mikono yake na kupiga kelele za kuomba msaada
wa kutaka kupewa maji ya kunywa.
Muda mfupi
baadaye alikata kauli (hakuweza kuongea tena) na kukaa kimya kama bubu.
Kufuatia
hali hiyo shuhuda alipiga kelele kuomba msaada kwa wananchi waliokusanyika na
kutaka kumuua wakidai kuwa vikongwe kama hao wamekuwa wakisumbua wananchi
kwa kuwaroga.
Hata hivyo
baada ya wananchi kufika na kutaka kumuua kwa kumchoma moto askari polisi wa
kituo kidogo kilichopo katika stendi hiyo waliweza kunusuru mama huyo na
kumpeleka katika Hospitali ya wilaya ya Geita kwa kuwa alikuwa ameumia
kichwani.
Mganga
Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Geita Adam Sijaona alikiri kumpokea mama
huyo na kuongeza kuwa ameumia kichwani kwa kuangukia jiwe lakini alikuwa
hajitambui wala alikuwa haongei na kulazwa wodi namba saba (7) kwa ajili ya
matibabu zaidi.
Jeshi la
Polisi Mkoani hapa limedhibitisha kutokea kwa tukio hilo na uchunguzi zaidi wa
tukio hilo unaendelea kubaini chanzo chake.
Na Valence
Robert-Malunde1 blog -Geita
|
No comments:
Post a Comment