SHEREHE ZA SERIKALI ZA MITAA:- Mkuu wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera Bw Richard Mbeho apiga marufuku tabia ya kunywa pombe nyakati za asubuhi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, July 03, 2014

SHEREHE ZA SERIKALI ZA MITAA:- Mkuu wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera Bw Richard Mbeho apiga marufuku tabia ya kunywa pombe nyakati za asubuhi.

Mkuu wa wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera, Bw.Richard Mbeho akikagua bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa kwa mikono kwa kutumia malighafi za kiasili na Wajasirimali wa wilaya hiyo wakati wa Sherehe za Serikali za Mitaa zilizfanyika kiwilaya katika kijiji cha Katoke, Kata ya Nyarubungo,hivi karibuni.


Muonekano wa Vikapu vilivyotengenezwa kwa mikono kwa kutumia malighafi za kiasili na Wajasirimali wa wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera .


Mkuu wa wilaya ya Biharamulo
Mkoani Kagera,Bw. Richard Mbeho.

Mkuu wa wilaya ya Biharamulo Mkoani Kagera Bw Richard Mbeho amepiga marufuku tabia ya wakazi wa wilaya hiyo kunywa pombe nyakati za asubuhi, badala yake watumie muda huo kufanya kazi ili kuchochea Maendeleo.

Akihutubia katika Mkutano wa Sherehe za Serikali za Mitaa zilizfanyika kiwilaya katika kijiji cha Katoke, Kata ya Nyarubungo, Bw Mbeho amesema unyaji wa pombe umekuwa kikwazo cha Maendeleo kutokana na baadhi ya wananchi kunywa pombe saa za kazi.

Amesema ni wajibu wa kila mwananchi kutumia muda wa Kazi kufanya shughuli za maendeleo badala ya kuanza kunyw apombe kuanzia asubuhi hadi jioni na wakati mwingine usiku wa manane ambapo amewataka viongozi wa vijiji na kata kuwashughulikia watu wa aina hiyo.

Katika Hatua nyingine Bw Mbeho amewataka Watumishi wa umma kuzingatia maadili huku Wenyeviti na Watendaji vijiji na kata wakitakiwa kuitisha mikutano na kuwasomea wananchi taarifa za mapato na matumizi.
 
Pia amewataka  wakazi wa wilaya hiyo kuhakikisha wanatunza akiba ya mazao ya nafaka na kuepuka kuyatumia kutengenezea Pombe ili kuepukana na Baa la njaa wilayani humo.


Wananchi  wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera, Bw.Richard Mbeho wakati wa Sherehe za Serikali za Mitaa zilizfanyika kiwilaya katika kijiji cha Katoke, Kata ya Nyarubungo,Hivi karibuni.
Habari Na:-Radio Kwizera FM-Ngara.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad