MAONESHO YA SABA SABA MKOANI KAGERA:-Tazama Bidhaa za Washiriki 255 kutoka ndani na nje ya nchi ya Tanzania katika maonesho ya sabasaba katika manispaa ya Bukoba. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, July 05, 2014

MAONESHO YA SABA SABA MKOANI KAGERA:-Tazama Bidhaa za Washiriki 255 kutoka ndani na nje ya nchi ya Tanzania katika maonesho ya sabasaba katika manispaa ya Bukoba.


Washiriki 255  kutoka ndani na nje ya nchi ya Tanzania  wamehudhuria  maonesho ya sabasaba katika manispaa ya Bukoba mkoani Kagera  katika kuuza na kununua bidhaa mbalimbali za wajasiliamali walioko katika jumuia ya Afrika Mashariki ambapo  Mmoja wa wafanyabiashara hao ,Bi.Elizabert  Ogake pichani amebainisha kuwa changamoto kubwa ni kupata usumbufu katika kuuza na kununua bidhaa kutoka mataifa jirani hasa wana pata misuko suko ya kutozwa ushuru wa bidhaa kutoka idara ya uhamiaji katika nchi ya Uganda.



Bi. Nasra Ally kutoka Nairobi Kenya akiwa katika maonesho ya sabasaba katika manispaa ya Bukoba mkoani Kagera. 



Ni Mzee  Charles Rugachwa kutoka Halmshauri ya Bukoba vijijini   mwenye fani ya uhunzi wa zana za kilimo cha Migomba  amewataka  wataalamu wa kilimo kudhibiti magonjwa ya migomba yanayoshambulia zao la  ndizi  kwa  wakulima kutumia zana bora za kilimo.


Wafanyabiashara kutoka nchini Kenya waliohudhuria maonesho ya sabasaba katika maispaa ya Bukoba mkoani Kagera wameitaka jumuia ya afrika ya Mashariki kuondoa vikwazo katika  mipaka ya nchi wanachama  ili kutoa fursa za masoko kwa jumuia hiyo

Mkurugenzi  wa  Shirika linalojihusisha  kukuza maendeleo ya kilimo na Biashara mkoani Kagera (KAIDEP) Bw Philmon Kamazima amesema katika  washiriki  hao ni kutoka katika mashirika , makampuni na taasisi mbalimbali za uzalishaji mali.

Bw Kamazima amesema kuwa kati ya wa washiriki hao 203 ni kutoka hapa nchini na 59 wametokea nchi za Uganda Kenya na Rwanda ambapo amesema katika maonesho hayo wanasisitiza ubora wa bidhaa na upanuaji wa masoko kimataifa.

Amesema katika ukuzaji wa uchumi kwa wananchi walioko katika  jumuia ya  Afrika Mashariki ni bora walio na makampuni na wafanya biashara wakubwa kuwekeza bidhaa zao na kupata sokola pamoja  ili kuongeza uzalishaji wa bidhaa .
  

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad