KOMBE LA DUNIA 2014:-'Kimbunga' cha mabao chapiga Brazil –Picha 13 Wakiikosa hata Nafasi ya 3. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, July 13, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014:-'Kimbunga' cha mabao chapiga Brazil –Picha 13 Wakiikosa hata Nafasi ya 3.

Timu ya Taifa ya Uholanzi imeibuka Mshindi wa 3 wa Kombe la Dunia 2014 baada ya Kuwachapa wenyeji wa fainali hizo Mwaka huu,Brazil bao 3 – 0,katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu Julai 12,2014.

Uholanzi walikwenda Mapumziko wakiwa mbele kwa bao 2-0 kwa magoli ya Robin Van Persie(penati dk 3),Daley Blind dk 17 huku Mchezaji Georginio Wijnaldum akikamilisha ushindi huo wa 3-0 dk ya 90.















Baada ya safari ndefu ya Mwezi mzima iliyoanzia Juni 12,2014, hapo Jumapili Julai 13,2014,Fainali za Kombe la Dunia Nchini Brazil zitafikia tamati huko Estadio Maracana, Jijini Rio de Janeiro Nchini Brazil, kwa Mechi ya Fainali ya Kombe la Dunia kati ya Germany na Argentina.

Germany imetinga Fainali hii kwa kishindo kikubwa kilichotikisa Dunia baada ya kuwabwaga Wenyeji wa Mashindano Brazil Jumanne iliyopita kwa kipondo cha Bao 7-1 huku wakifunga Bao zao 5 za kwanza ndani ya Dakika 29 na Bao lao la Pili hadi la 5 yakipigwa ndani ya kipindi cha Dakika 6 tu.

 

Argentina walipata msukosuko kwenye Nusu Fainali yao na Netherlands kwa kwenda Dakika 120 wakiwa Sare 0-0 na hatimae kufuzu kwa Mikwaju ya Penati 4-2 hapo Jumatano.

 

Fainali hii ya Jumapili inakumbushia Fainali za Miaka ya 1986 na 1990 miamba hii ilipopambana.

 

Fainali hizo ndizo mara ya mwisho kwa Nchi hizo kutwaa Kombe la Dunia wakati Argentina ilipoifunga West Germany huko Mexico Mwaka 1986 na Germany kuifunga Argentina Mwaka 1990 na kuwa Mabingwa wa Dunia.

 

Tangu wakati huo, Argentina na Germany hazijatwaa tena Kombe la Dunia.


Katika michuano hii ya 20 jumla ya zawadi ambazo hutolewa kwa timu shiriki 32 ni kiasi cha dola za Kimarekani, millioni 576. 

Vilabu vya Brazil vimepata kiasi cha dola millioni 70. Asilimia 37 ya kiwango cha pesa katika zawadi kimeongezeka kutoka katika michuano ya mwaka 2012 nchini Afrika Kusini. Kabla ya michuano kuanza kila timu ilipewa kiasi cha dola millioni 1.5 kwa ajili ya maandalizi.
 

 FIFA imegawanya zawadi hizo katika mafungu saba tofauti huku bingwa wa michuano akipata kiasi cha juu zaidi. 

 

Dola millioni nane zilitoka kwa timu 16 ambazo ziliondoshwa katika michuanohatua ya awali.

 

Timu ambazo zilipata mgawo huo ni kama Cameroon, Ivory Coast, Ghana, Iran, Korea Kusini,Australia, Japan,Croatia, Bosnia, England, Italia, Hispania, na nyingine zilizoishia hatua ya awali hivyo ukitoa matokeo mabaya kwa timu hizo zilipata pesa ya kutosha.

 

 Kundi la pili la zawadi ni lile ambalo linahisha timu 16 ambazo zilifuzu kwa hatua ya 16 bora. 

 

Kiasi cha dola millioni tisa kilitolewa kwa kila timu ambayo ilishindwa katika mchezo wa hatua hiyo na kuondolewa mashindanoni.

 

Mexico, Chile, Uruguay, Algeria,Nigeria, Uswizi, Marekani na Ugiriki ndizo zilipata kitita hicho. Dola millioni 14 zilitolewa kwa timu nne ambazo zilishindwa katika michezo ya robo fainali.

 

Ufaransa, Colombia,Costa Rica na Ubelgiji ndiyo zilinufaika na malipo hayo. Timu ambazo zilishindwa katika nusu fainali zitapambana ili kupata washindi wa tatu na yule wa nne.

 

Timu itakayofungwa katika mchezowa kutafuta mshindi wa tatu katika ya Brazilna Uholanzi itapata kiasi cha dola millioni 20. Mshindi wa tatu atapata kiasi cha dola millioni 22.

 

Mshindwa katika mchezo wa fainali atapata kiasi cha dola millioni 25, na bingwa ataondoka na kiasi cha juu zaidi., dola za KImarekani millioni 35.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad