HUDUMA KWA WANANCHI:-*Soma Mapendekezo kuhusu kugawanywa kwa Jimbo la uchaguzi la Ngara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, July 25, 2014

HUDUMA KWA WANANCHI:-*Soma Mapendekezo kuhusu kugawanywa kwa Jimbo la uchaguzi la Ngara.

Ni muonekano wa Mlima/Pori ambalo lilikutwa limechomwa moto na Watuwasiojulikana katika Kijiji cha Kasharaji wilayani Ngara mkoani Kagera huku juhudi za kudhibiti uchomaji moto hovyo unaoharibu Mazingira na hata Kuharibu Miti iliyopandwa katika Viwanja likisuasua.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Mkoani Kagera Bw Cornel Ngudungi amesema mapendekezo kuhusu kugawanywa kwa Jimbo la uchaguzi la Ngara yatatolewa kwenye kikao kijacho cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo.

Bw Ngudungi ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akijibu swali la diwani wa Kata ya Bugarama Bw Adroniz Bulindoli wakati wa maswali ya Papo kwa Papo katika kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Ngar.

Amesema suala hilo tayari limejadiliwa kwenye kikao cha CMT na kwamba mapendekezo ya kugawanya Jimbo hilo la uchaguzi yatatolewa rasmi kwenye kikao kijacho cha Baraza la Madiwani.

Awali Bw Bulindoli ameshauri Jimbo la Uchaguzi la Ngara ligawanywe ili yapatikane majimbo mawili ambayo ni Ngara Kusini na Ngara Kaskazini kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi kutokana na ukubwa wa Jimbo la sasa pamoja na idadi ya watu waliopo.

Habari Na:-Radio Kwizera-Ngara.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad