PICHA /SOMA:-Tazama Yaliyojiri wakati Ngara Stars ikifunga bao 1-0 Bandari Biharamulo katika kuwania Mazagazaga Cup 2014-Nyakanazi,wilayani Biharamulo mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, June 01, 2014

PICHA /SOMA:-Tazama Yaliyojiri wakati Ngara Stars ikifunga bao 1-0 Bandari Biharamulo katika kuwania Mazagazaga Cup 2014-Nyakanazi,wilayani Biharamulo mkoani Kagera.

Kikosi cha Ngara Stars katika picha ya pamoja kwenye uwanja wa Nyakanazi shule ya Msingi ,kushoto kabisa ni Baraka Abas ambae ni Timu Meneja na kulia ni Kocha mkuu Seleman Ally aka Mzanzibar wakati waliposhuka dimbani kuwavaa Bandari Biharamulo May 31,2014.


Kikosi cha Bandari Biharamulo kilichofungwa bao 1-0 na Ngara Stars kwenye mchezo wa kuwania Mazagazaga Cup 2014.

Muonekano wa uwanja wa Shule ya Msingi Nyakanazi unaotumiwa kushindana timu kuwania Kombe la Mazagazaga 2014 ,likiwa na thamani ya shilingi Laki 8 kwa mshindi wa Kwanza atakayelinyakuwa.





Mfungaji wa goli la Ngara Stars  Wise Khalifa Mohamed mwenye chupa ya maji akifunga bao hilo Moja kwa  kichwa akiunganisha mpira wa adhabu uliopigwa na Kipa wa Bandari kuutema.


Picha juu ni Mashabiki wa Ngara Stars waliosafiri na timu hiyo kutoka wilayani Ngara mkoani Kagera hadi Nyakanazi kuishangilia ,mwenyeflana nyekundi ni Timu meneja wa Ngara Stars Baraka Abas wakifatilia mchezo kati ya Ngara Stars dhidi ya Bandari Biharamulo katika uwanja wa Nyakanazi shule ya msingi May 31,2014.


Ikisafiri hadi Nyakanazi,wilayani Biharamulo mkoani Kagera,Timu ya Ngara Stars imefanikiwa kujiongezea point 3 muhimu katika harakati zake za kuwania kombe la Mazagazaga 2014 baada ya kuifunga timu ya Bandari kutoka Biharamulo bao 1-0.

Goli hilo la Ngara Stars lilifungwa na Mchezaji wake Wise Khalifa Mohamed baada ya kufunga kwa kichwa akiunganisha mpira wa adhabu uliopigwa na Kipa wa Bandari kuutema.

Kwa ushindi huo sasa Ngara Stars imefikisha point 4 katika kundi lao la C la Mazagazaga CUP 2014 zikiwemo pia timu za Polisi Kibondo,Cobra ya Masumbwe,Nyakanyasi ya Bukoba na Bandari ya Biharamulo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad