SOMA / KUJITOA UHAI:-Mahakama yamhukumu kifungo cha miaka miwili jela baada ya mshtakiwa kukiri kosa la kutaka kujiua kwa kujinyonga-Wilayani Ngara mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, May 27, 2014

SOMA / KUJITOA UHAI:-Mahakama yamhukumu kifungo cha miaka miwili jela baada ya mshtakiwa kukiri kosa la kutaka kujiua kwa kujinyonga-Wilayani Ngara mkoani Kagera.


…’’..Mshtakiwa alifanya kosa hilo May 22 ,2014, ambapo alitaka kujiua kwa kujinyonga kabla ya kuokolewa na mtu aliyemuona akifanya jaribio hilo….’’Picha Na Maktaba Yetu.
Mahakama ya wilaya ya Ngara Mkoani Kagera imemhukumu kifungo cha miaka miwili jela mkazi wa kijiji cha Mubinyange wilayani Ngara, baada ya mshitakiwa huyo kukiri kosa la kutaka kujiua kwa kujinyonga.

Hakimu wa Makahama ya wilaya ya Ngara Bw. Andrew Kabuka amesema mahakama hiyo imemtia hatiani Mshtakiwa Cyprian Msigwa mwenye umri wa miaka 32 baada ya kukiri kosa la kutaka kujiua mwenyewe.

Hakimu Kabuka amesema Mahakama hiyo imeridhika na maelezo aliyoyatoa mshitakiwa kuwa alitaka kujiua kutokana na kuudhiwa na mtu na kwamba ni kosa la jinai mtu kujitoa uhai, na hivyo Mahakama kumtia hatiani na kumhukumu kifungo cha miaka miwili jela.

Awali, Mwendesha Mashitaka wa polisi Bw George Gorotto ameiambia mahakama kuwa mshtakiwa alifanya kosa hilo May 22 mwaka huu, ambapo alitaka kujiua kwa kujinyonga kabla ya kuokolewa na mtu aliyemuona akifanya jaribio hilo.

Habari Na:-Radio Kwizera FM.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad