SOMA:-Kifo cha Meneja EWURA- Familia yamwachia Mungu…Mazishi yake ni Leo(May 22,2014)Kijijini kwao Murukulazo Ngara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, May 22, 2014

SOMA:-Kifo cha Meneja EWURA- Familia yamwachia Mungu…Mazishi yake ni Leo(May 22,2014)Kijijini kwao Murukulazo Ngara.

Mwili wa Julius Gashaza ukiwa katika jeneza ambapo leo (May 22, 2014) saa 4:00 asubuhi utapelekwa katika Kanisa la Anglikana katika kijiji cha Murukulazo kwa ajili ya sala na saa 6:00 mchana utaagwa kabla ya mazishi yatakayofanyika nyumbani kwake.

Meneja Biashara ya Petroli wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) nchini Tanzania, Julius Gashaza enzi za uhai wake.

Hii ni Hoteli aliyodaiwa kulala Meneja huyo wa Ewura.

.......Chumba alichodaiwa kulala Meneja wa Ewura.......

..................Hiki ni choo alichokutwa meneja huyo............

....Meneja Gashanza (mwenye kofia) akiwa kazini enzi za uhai wake........


Aliyekuwa Meneja wa Biashara ya Petroli wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), Julius Gashaza anazikwa leo (May 22, 2014) katika Kijiji cha Murukulazo, wilayani Ngara mkoani Kagera huku familia yake ikisema haina cha kusema kuhusu kifo hicho, bali inamwachia Mungu.

Akizungumza  kijijini hapo, mdogo wa marehemu, Alex Gashaza alisema familia imepokea msiba huo kwa mshtuko mkubwa na kushangazwa na taarifa kwamba ulitokana na kujinyonga kama inavyodaiwa.

Alisema baada ya kupokea simu kutoka Dar es Salaam kuhusu mazingira ya kifo hicho, wameshindwa kujua sababu za kifo kwa kuwa hakuna mtu aliyezungumza naye.

Alisema kaka yake hakuwa na tatizo lolote na wanafamilia, ndugu wala jamaa zake wa karibu, hivyo familia haiwezi kuelezea jambo ambalo halina ushahidi, badala yake inaacha tukio hilo mikononi mwa Mungu.

Mwili wa Gashaza baada ya kuwasili Murukulazo jana (May 21,2014) jioni na leo saa 4:00 asubuhi utapelekwa katika Kanisa la Anglikana katika kijiji hicho kwa ajili ya sala na saa 6:00 mchana utaagwa kabla ya mazishi yatakayofanyika nyumbani kwake.

Kiongozi wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Victoria Nyanza mkoani Mwanza, Mchungaji Lazaro Manjelenga ambaye pia ni baba mkwe wa mdogo wa marehemu, alisema wana matumaini na Muumba kwa kile kilichotokea.

“Siri ya Mungu na mwanadamu wake hakuna wa kuijua, hivyo tusihukumu,” alisema na kuongeza kuwa mazishi yatafanyika kwa mujibu wa taratibu za Kanisa hilo.

MASWALI  MATANO KIFO CHA MENEJA EWURA.

Swali la kwanza:- Kama kweli marehemu alinyongwa ni kwa nini mlango ulikutwa umefungwa kwa ndani? Je, mnyongaji alitokaje baada ya kutekeleza mauaji hayo?

Swali la pili:- Kama kweli marehemu alinyongwa, kwa nini kitandani kulikutwa na alama ya mtu kukaa tu na kusiwepo kwa dalili za mapambano au purukushani?

Swali na tatu:- Kama kweli alijinyonga mwenyewe ni kwa nini iwe kipindi hiki ambacho inadaiwa alipokea vitisho kutoka kwa wabaya wake kwamba atauawa?

Swali la nne:- Uamuzi wa kuchukua chumba kwenye hoteli hiyo ulitoka kwa nani? Marehemu mwenyewe au? Kama alishauriwa, aliyemshauri ana cha kujibu?

Swali la tano:- Kama kulikuwa na matatizo ya kikazi kama ilivyodaiwa, basi Mkurugenzi Mstaafu wa Ewura, Haruna Masebu atakuwa anayajua hivyo angeweza kusaidia kuyasema.

Swali lingine ambalo lingeweza kuongeza idadi ni juu ya uwezekano wa kuingizwa kwa funguo nje wakati ya ndani ilizungushwa lakini imebainika kwamba baada ya funguo kufungwa na mlango kuwa ‘lokdi’, funguo hiyo huwa ‘luzi’ tena hivyo mwenye funguo nje anaweza kuisukuma na kuingiza nyingine.


Aidha tayari Jeshi la Polisi limeunda jopo la Upelelezi kuchunguza kifo hicho cha Gashaza kinachodaiwa kutokea katika mazingira ya kutatanisha na kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam,Suleiman Kova alisema kuwa Jopo hilo litaongozwa na Mkuu wa Upelelezi kanda hiyo Jaffar Mohamed akishirikiana na wataalamu wa Maabara kuu ya Polisi,Daktari Bingwa wa Polisi na Serikalini.

Kamanda Kova amesema jeshi hilo linafanya uchunguzi ili kuoandoa utata ulioanza kujitokeza kuhusiana na kifo chake baada ya taarifa kuzaga kwamba kilitokana na kutoelewana na Viongozi wenzake katika Masula ya kikazi.

Alisema uchunguzi huo ukikamilika ,Jalada litapelekwa kwa Mwanasheria mkuu wa Serikali ili hatua za kisheria zichukuliwe.
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad