SHUKRANI YA MASHUJAA BANDI KUBEBA TUZO 8:- Sasa Kufanya ziara katika Mikoa yote ya Tanzania....'' - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, May 23, 2014

SHUKRANI YA MASHUJAA BANDI KUBEBA TUZO 8:- Sasa Kufanya ziara katika Mikoa yote ya Tanzania....''


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa bendi ya muziki wa Dansi ya Mashujaa Maximillian Luhanga (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari May 22,2014 kuhusu ziara yao itakayofanyika katika mikoa yote Tanzania baada ya mfungo wa Mwezi wa Ramadhan pamoja na kutoa shukrani kwa wapenzi wao kwa kuwapa tuzo 8 kwa miaka 2 …..kutoka kushoto ni Raja Ladha na King Dodoo  kulia.

Bendi  ya muziki wa dansi nchini Tanzania Mashujaa, inatarajia kufanya ziara katika mikoa yote nchini nzima kwa ajili ya kutoa shukrani kwa mashabiki wao waliowapigia kura kwenye tuzo za Kilimanjaro Music Awards.

Akizungumza Dar es Salaam jana (May 22,2014) , Mkurugenzi wa Mawasiliano wa bendi hiyo Maximillian Luhanga, alisema kuwa wamepata mafanikio makubwa kwa miaka miwili baada ya kupata tuzo nane.

Alisema kuwa mwaka jana (2013) walipata tuzo tano na mwaka huu ( 2014) wamefanikiwa kupata tuzo tatu kutokana na kura za mashabiki wao.


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa bendi ya muziki wa dansi ya Mashujaa Maximillian Luhanga (kulia) akizungumza na Waandishi wa Habari jana kuhusu ziara yao itakayofanyika katika mikoa yote baada ya mfungo wa Mwezi wa Ramadhan, kustoto ni rapa wa bendi hiyo Raja Ladha.
Alisema kuwa wamejifunza mambo mengi katika muziki kutokana na kuwa wanakubali ushauri kutoka kwa mashabiki wao.

Tunatarajia kufanya ziara katika mikoa yote ya Tanzania baada ya kupata tuzo tatu mwaka huu na hivyo hiyo ziara itakuwa kwa ajili ya kuwashukuru mashabiki wetu,” alisema.

Alisema kuwa wamesharekodi nyimbo mbili mpya ambazo watazitumia mikoani ikiwa ni kama zawadi kwa mashabiki wao, ambapo nyimbo hizo ni Usidharau Sifuri na Kiu ya Haki.

Alisema kuwa ili waendelee kuwa karibu na mashabiki wao kila mwezi watakuwa wanatengeneza matukio mbalimbali ya bendi katika mitandao ya Kijamii.

KUPATA HABARI / NYIMBO KUHUSU MASHUJAA BAND INGIA HAPA ZAIDI>>>>>https://www.facebook.com/mashujaaband?fref=ts
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad