Viongozi hao pamoja na Wanamichezo 577,wanawake wakiwa 268 kwa pamoja na watazamaji waliojitokeza waliimba nyimbo za Kizalendo ukiwemo wa AMANI NA MAENDELEO mkoani Kagera.
|
....................wakiimba....Amani na Maendeleoo.........Kagera...............
|
Mashindano
ya michezo kwa umoja wa shule za sekondari Ngazi ya mkoa kwa Mkoa wa Kagera
yamezinduliwa rasimi leo jumamosi May 24, 2014 na mkuu wa Mkoa wa Kagera,Kanal
mstaafu Fabiani Masawe.
Akifungua
mashindano hayo yanayofanyika katika viwanja vya chuo cha ualimu katoke
wilayani Muleba,Kanali Massawe amesema kuwa licha ya azma ya Serikali
kutekeleza sera ya michezo nchi,wakati umefika sasa kwa Wakuu wa wilaya na
Wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya mkoani humo nao kuhudhuria Mashindano hayo
ya UMISETA ili kuwa chachu ya kuendeleza
michezo katika wilaya zao.
Katika hatua
nyingine Mkuu huyo wa mkoa wa Kagera –Fabiani Masawe amewataka washriki wa
mashindano ya UMISETA kwa mwaka huu kuonyesha nidhamu na bidii wakati wa
mashindano ili vipaji vyao vionekane na kuendelezwa.
Awali
akimkaribisha Mgeni rasimi katika ufunguzi huo,Makamu mwenyekiti wa UMISETA
mkoa wa Kagera na Mwenyekiti wa UMISETA wilaya ya Ngara-Julius Nestori amesema
kuwa mashindano hayo kwa mwaka huu yanashirikisha yanashirikisha wanamichezo
577 kutoka wanafunzi waliochaguliwa katika shule za sekondari za wilaya 8 za
mkoa wa Kagera na yana lengo la kupata timu ya UMISETA mkoa wa Kagera.
Wilaya hizo
ni Manispaa,Bukoba Vijijini,Karagwe,Kyerwa,Misenyi,Ngara,Biharamulo na Muleba.
Mara baada
ya ufunguzi-Timu ya soka ya UMISETA ya Halmashauri ya wilaya ya Ngara iliingia
dimbani kupambana na wenzao wa Kyerwa katika uwanja wa soka wa chuo cha Katoke
na kufanikiwa kuwafunga bao 2-1 magoli ya ushindi ya Ngara yakifungwa na Antoni
Oscar na Maziku Katika mchezo wa soka la wanawake,Timu ya soka ya UMISETA ya
Halmashauri ya Bukoba iliwanyanyasa
vilivyo wenzao wa Biharamulo kwa kuwatandika magoli 6-0.
Mwenyekiti
wa UMISETA au Afisa Michezo mkoa wa Kagera-Khepa Eliasi amesema kuwa UMISETA
ngazi ya kikanda ili kupata timu ya ZIWA MAGHARIBI- sasa itafanyika katika
viwanja vya chuo cha ualimu Katobe kuanzia May 31,2014 badala ya Geita kama
ilivyokuwa imepangwa hapo awali.
No comments:
Post a Comment