VPL 2013/2014:- April 19, 2014,Ni mechi za Mwisho wa Msimu-Yanga SC v/s Simba SC –Ashanti au Prisons nani kushuka huku Azam FC kudumisha kutofungwa..’’ - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, April 18, 2014

VPL 2013/2014:- April 19, 2014,Ni mechi za Mwisho wa Msimu-Yanga SC v/s Simba SC –Ashanti au Prisons nani kushuka huku Azam FC kudumisha kutofungwa..’’


Azam FC ilifanikiwa kujihakikishia taji la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara 2013/2014, baada ya kuifunga Mbeya City mabao 2-1 na kufikisha pointi 59 ikiwa na mchezo mmoja wa kufunga pazia la Ligi Kuu Jumamosi(April 18, 2014) dhidi ya JKT Ruvu Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam na siku hiyo itawania kuvunja rekodi ya Simba SC na Pan Africans kutwaa ubingwa wa ligi hiyo pasipo kupoteza mechi.

Ligi kuu soka Vodacom Tanzania bara ,msimu wa 2013/2014, inafikia tamati yake Jumamosi Aprili 19,2014, na Mechi zote ni za kukamilisha Ratiba tu kasoro ile itakayochezwa huko Uwanja wa Jamhuri, Morogoro kati ya Ashanti United na Tanzania Prisons ambayo itaamua nani wanaungana na JKT Oljoro na Rhino Rangers kucheza Daraja la Kwanza, FDL, Msimu ujao wa 2014/2015.

Hali hii ni kwamba tayari Bingwa ameshapatikana ambae ni Azam FC na Timu ya Pili ni Yanga SC.

Lakini pia ipo Mechi tamu kwa Mashabiki wa Kandanda Tanzania na si nyingine bali ni ile Dabi ya Kariakoo inayokutanisha Miamba ya Soka, Yanga SC na Simba SC, ambazo zikikutana hamna masihara ni kazi kweli kweli na vidole machoni.

Timu hizi zilitoka Sare ya Bao 3-3 katika Mechi yao ya Kwanza ya Ligi ambapo Yanga SC waliongoza 3-0 hadi Mapumziko na Simba SC kusawazisha Bao zote Kipindi cha Pili.

Baada ya hapo, Yanga SC na Simba SC zilikutana Mwezi Desemba,2013 kwenye lile pambano la Nani Mtani Jembe na Simba SC kuibuka kidedea kwa Bao 3-1.

Pia wale Wadau safi wa Soka watataka kujua ikiwa Mabingwa wapya, Azam FC, ambao wamefuta mwiko wa Yanga SC na Simba SC kupokezana Ubingwa tangu Mwaka 2000 walipochukua Mtibwa Sugar kwa mara ya mwisho, wataweza kudumisha Rekodi yao murua ya kutofungwa Mechi hata moja ya Ligi Msimu huu watakapofunga dimba dhidi ya JKT Ruvu huko Azam Complex, Chamazi, Viunga vya Jiji la Dar es Salaam.

LIGI KUU VODACOM TANZANIA BARA 2013/2014.

Mechi za mwisho za Ligi

Jumamosi Aprili 19,2014.

Rhino Rangers v Ruvu Shooting [Ali Hassan Mwinyi, Tabora]

Mbeya City v Mgambo JKT [Sokoine, Mbeya]

Tanzania Prisons v Ashanti United [Jamhuri, Morogoro]

JKT Ruvu v Azam FC [Azam Complex, Chamazi]

JKT Oljoro v Mtibwa Sugar [Sheikh Amri Abeid, Arusha]

Coastal Union v Kagera Sugar [Mkwakwani, Tanga]

Yanga v Simba [National Stadium, Dar es Salaam]

MSIMAMO VPL 2013/2014.

NA TIMU P W D L F A GD PTS
1  Azam FC 25 17 8 0 50 15 35 59
2  Young Africans 25 16 7 2 60 18 42 55
3 Mbeya City 25 12 10 3 32 20 12 46
4 Simba SC 25 9 10 6 40 26 14 37
5 Kagera Sugar 25 8 11 6 22 20 2 35
6 Ruvu Shooting 25 9 8 8 26 32 -6 35
7 JKT Ruvu 25 10 1 14 23 39 -16 31
8 Mtibwa Sugar 25 7 9 9 29 30 -1 30
9 Coastal Union 25 6 11 8 16 19 -3 29
10 Mgambo JKT 25 6 8 11 18 34 -16 26
11 Tanzania Prisons 25 5 10 10 25 33 -8 25
12 Ashanti United 25 6 7 12 20 38 -18 25
13 JKT Oljoro 25 3 9 13 18 36 -18 18
14 Rhino Rangers 25 3 7 15 18 37 -19 16

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad