VPL 2013/2-14:-Azam FC Bingwa wa Tanzania bara tangu wamepanda ligi kuu msimu wa 2008/2009. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, April 14, 2014

VPL 2013/2-14:-Azam FC Bingwa wa Tanzania bara tangu wamepanda ligi kuu msimu wa 2008/2009.



Klabu ya Azam FC imefanikiwa kuweka rekodi mpya kwa kutwaa ubingwa wa Tanzania bara kwa mara ya kwanza ambapo iliukosa ubingwa huo mara mbili mfululizo ikishika nafasi ya pili.

RASMI Azam FC wamefanikiwa kutwaa Ubingwa wa Ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2014 baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City FC kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Kwa matokoe hayo, Azam FC wamefikisha pointi 59 kileleni ambazo haziwezi kufikiwa na klabu yoyote ile, huku wakiwa na mchezo mmoja mkononi.


Baadhi ya Wachezaji wa Mbeya City,
Wakimuandama Mwamuzi wa mechi yao
Na Azama FC waliyolala 2-1,
Jana(April 13,2014)
Taarifa kutoka Mbeya zinaeleza kuwa mechi iliingia dosari baada ya wachezaji wa Mbeya City kumshambulia mwamuzi kutokana na kutoridhishwa na maamuzi yake.

Mbeya City baada ya kuchapwa jana(April 13,2014), wanabakia katika nafasi ya tatu kwa pointi 47 na rasmi wameshajiengua kutafuta nafasi ya tatu kwa sababu hata kama watashinda mechi yao ya mwisho dhidi ya Mgambo JKT aprili 19,2014, watafikisha pointi 50 ambazo zimepitwa na Yanga SC.

Kwa mazingira hayo, Mbeya City wameshika nafasi ya tatu, Yanga SC ya pili na Azam FC ni mabingwa wapya.

Yanga SC waliokuwa wanafukuziana na Azam FC kuwania ubingwa wameshinda mabao 2-1 dhidi ya JKT Oljoro katika dimba la Shk. Amri Abeid jijini Arusha, lakini ushindi huo haujawasaidia chochote kutokana na ushindi wa Azam FC jana(April 13,2014).

Yanga SC wamefikisha pointi 55, pointi nne nyuma ya Azam FC, huku timu zote zikisaliwa na mechi moja moja mkononi.

Hata kama Yanga SC watashinda mechi ya mwisho Aprili 19,2014, uwanja wa Taifa dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Simba SC hawataweza kufikia pointi 59 walizonazo Azam FC.

Mabingwa wapya wa Ligi kuu, Azam FC watafunga pazia dhidi ya Maafande wa JKT Ruvu ambao kwa asilimia zote wamefanikiwa kukwepa kushuka daraja baada ya ushindi wa bao 1-0 walioupata jana katika dimba la Mkwakwani dhidi ya Coastal Union.

Mechi nyingine muhimu jana(April 13,2014) ilipigwa katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam ambapo Wekundu wa Msimbazi Simba SC waliwakaribisha Wauza Mitumba wa Ilala, Ashanti United.

Mechi hiyo imemalizika kwa kocha Abdallah Kibadeni kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mcroatia wa Simba sc, Dravko Logarusic.

Kwa matokeo hayo, Ashanti United wanapata unafuu wa kusalia ligi kuu, huku wakisubiri mechi ya mwisho dhidi ya Prisons aprili 19 mwaka huu uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro.

Sasa Ashanti wamefikisha mechi 25 na kujikusanyia pointi 25 sawa na Prisons walioshinda mabao 4-3 jana dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora, lakini Wajelajela wanakuwa juu yao kutokana na wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Kwa kutwaa Ubingwa huku wakiwa na Mechi 1 mkononi, Azam FC imefuta kuhodhi kwa Ubingwa kwa Vigogo Yanga na Simba tangu Mwaka 2001 ambapo, baada ya Mtibwa kuutwaa Mwaka 2000 na kuutetea Mwaka 2001, Yanga na Simba zimekuwa zikipishana kwa kuubeba.

MABINGWA WALIOPITA LIGI KUU SOKA TANZANIA BARA.

1965 Sunderland (Sasa ni Simba SC)

1966 Sunderland

1967 Cosmopolitan

1968 Young Africans

1969 Young Africans

1970 Young Africans

1971 Young Africans

1972 Young Africans

1973 Simba SC

1974 Young Africans

1975 Mseto SC

1976 Simba SC

1977 Simba SC

1978 Simba SC

1979 Simba SC

1980 Simba SC

1981 Young Africans

1982 Pan Africans

1983 Young Africans

1984 Simba SC

1985 Young Africans

1986 Tukuyu Stars

1987 Young Africans

1988 Coastal Union

1989 Young Africans

1990 Simba SC

1991 Young Africans

1992 Young Africans

1993 Young Africans

1994 Simba SC

1995 Simba SC

1996 Young Africans

1997 Young Africans

1998 Young Africans

1999 Mtibwa Sugar

2000 Mtibwa Sugar

2001 Simba SC

2002 Young Africans

2003 Simba SC

2004 Simba SC

2005 Young Africans

2006 Young Africans

2007 Simba SC

2007/08 Young Africans

2008/09 Young Africans

2009/2010 Simba SC

2010/2011 Young Africans

2011/2012 Simba SC

2012/2013 Young Africans

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad