Amezaliwa
mkoa wa Pwani wilaya ya Kisarawe 1940. Elimu ya Msingi alisoma katika Shule ya Pugu kuanzia darasa la kwanza mpaka
la tatu, mwaka 1956, mjomba wake aliamua kumuamishia Dar es Salaam ambako alisoma zaidi elimu ya
dini 'Kuran', Mtaa wa Lindi, Ilala.
Gurumo
aliyezaliwa mwaka 1940, alianza muziki mwaka 1960 katika bendi ya Kilimanjaro
Chacha, mwaka 1962 akajiunga na Rufiji Jazz Band, kabla ya kutua Kilwa Jazz
mwaka 1963.
Mwaka 1978
aliamia Mlimani Park Orchestra na mwaka 1985 alijiunga na Bendi ya Orchestra Safari Sound (OSS-
Ndekule) lakini siku zote maisha yake
yamekuwa Msondo ambayo ndiyo bendi iliyopitia majina ya Nuta, Juwata na Ottu.
Ndugu wa marehemu
Gurumo
wakiwa
katika picha ya pamoja,
kuanzia
kushoto ni mtoto wake Mwalimu Muhidin,
Mariamu Muhidin na Omari Muhidin
anayefuatia
ni kaka wa marehemu
Bw.Ramadhani
Mwishehe.
|
Tangu miaka
ya 1960 kama ungethubutu kutamka humjui Gurumo, ungeonekana mshamba ambaye
tasnia ya muziki umeipa kisogo,alikuwa staa mkubwa sana wa muziki kipindi hicho
ingawa jina lake limebaki juu kuanzia
nyakati hizo mpaka sasa.
Ni kamanda
hodari, aliyeifanya Bendi ya Msondo ‘Msondo Ngoma’ ipate heshima kubwa mpaka
ikaitwa Baba ya Muziki Tanzania(Msondo na sasa Msondo Ngoma Music Band, bendi
aliyodumu nayo hadi kifo chake licha ya kuchomoka mwaka 1978 kwenda kuanzisha
DDC Mlimani Park ‘Sikinde).
Tungo zake
nyingi ni lulu ambayo haitafutika kamwe. Kinachoumiza kwa sasa ni kuona Gurumo
hawezi tena kusimama jukwaani.
Mzee huyo
ndiye aliyeivusha Msondo kupitia majina
ya Nuta, Juwata, na Ottu, ikiwa
inamilikiwa na Chama cha Wafanyakazi.
Itambulike
kuwa yeye akiwa na wenzake kama marehemu Shaaban Mhoja Kishiwa maarufu kama ‘TX Moshi William’, Saidi
Mabera, marehemu Suleiman Mbwembwe, Othuman Momba, Joseph Maina na wengineo,
ndiyo waliounganisha nguvu na kuimiliki, baada ya chama cha wafanyakazi
kujiondoa katika uendeshaji wa bendi.
Maalim
Muhidin Gurumo ,
enzi za uhai
wake.
|
Gwiji huyo
wa muziki aliyeanza kuimba mwaka 1960, atakumbukwa na nyimbo zake zenye kubeba
ujumbe kulingana na mazingira husika iwe siasa, uchumi na masuala ya kijamii.
Agosti mwaka
jana, Mzee Gurumo alitangaza kustaafu muziki baada ya kuitumikia fani hiyo kwa
miaka 53.
Alifanya
hivyo kutokana na umri na afya yake kuzorota mara kwa mara kwa sababu ya
maradhi.
Ameimba
zaidi nyingi zikiwamo za Usimchezee Chatu, Selina piga moyo konde na nyinginezo
nyingi, huku akiwa pia mwalimu wa wanamuziki wengi mahiri nchini.
No comments:
Post a Comment