SOMA:-Tangazo La Usaili April 2014,kwa Walioomba Kazi Serikalini. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, April 29, 2014

SOMA:-Tangazo La Usaili April 2014,kwa Walioomba Kazi Serikalini.

Wasailiwa walioitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia yafuatayo:-

 1. Ukaguzi wa vyeti utafanyika saa 1:00 kabla ya muda wa mtihani wa mchujo kuanza. 

2. Kwa wale wasiokuwa na mtihani wa mchujo usaili utaanza saa moja kamili asubuhi (1:00) na utafanyika mahali na tarehe kama inavyoonesha katika nafasi husika. 

3. Kuja na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi mfano: kitambulisho cha mkazi, kupigia kura, kazi, hati ya kusafiria n.k 

4. Kuja na Vyeti Halisi (original certificates) vya kuanzia kidato cha nne, sita, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za mwombaji. 

5. “Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA. 

6. Kila msailiwa aje na picha moja (Passport size). 

7. Kila msailiwa atajigharamia kwa chakula, usafiri na malazi.

8. Kila msailiwa azingatie tarehe na eneo alilopangiwa kufanyiwa usaili 

9. Kila msailiwa aje na cheti halisi cha kuzaliwa (Original Birth Certificate)

10. Kwa wale waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na mamlaka husika (TCU & NECTA)
 
11. Wale ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa maombi yao hayakufanikiwa na wasisite kuomba tena mara nafasi za kazi zitakapotangazwa. 

12. Kada zenye mchujo, wasailiwa watakaofaulu mtihani wa mchujo wazingatie mahali na tarehe za usaili wa mahojiano kama ilivyooneshwa kwenye tangazo. 


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad