![]() |
|
Kikosi cha Timu
ya Kumunazi FC,licha ya kucheza soka safi na la kuvutia lakini kilikubali kupoteza mchezo wao huo wa fainali dhidi ya Benaco Stars March 30,2014 mjini Benaco.
|
![]() |
|
Waamuzi wa mchezo huo wa fainali kati ya Benaco Stars na Kumunazi FC walikuwa ni Ramadhani Makule,Rwegasira Kashunja na Abdul Mwandik.
|
![]() |
|
Diwani wa
kata ya Kasulo Philbert Kiiza alikua mgeni rasmi na alipata fursa ya kuzikagua timu zote mbili na kuwataka kucheza mchezo safi kwa kuacha fujo na jazi sambamba na kuzingatia fair play.
|
![]() |
|
Wanne kutoka kushoto ni mwakilishi
wa Mdhamini wa Ligi ya Makoye-2014 kata ya Kasulo, Costantine Morandi amesema kuwa mashindano hayo yatakuwa endelevu kwa
kuchezwa kila Mwaka katani humo.
|
![]() |
|
Mgeni rasmi Diwani Philbert Kiiza akizungumza na timu zote mbili mara baada ya kuzikagua.
|
![]() |
|
Mashabiki mablimbali wakifatilia mchezo huo wa fainali katika uwanja wa Benaco ambapo Benaco Stars ilifanikiwa kuibuka Bingwa wa Ligi ya Makoye 2014,kwa ushindi wa bao 2-1.
|
![]() |
|
Muonekano wa uwanja wa Benaco licha ya timu kucheza soka safi na la kuvutia ,ila uwanja uliwaathiri wachezaji kwa kujaa tope na kuteleza kwa sababu ya
mvua kunyesha kabla ya mchezo.
|
![]() |
|
Benchi la
Ufundi la Timu ya Benaco Stars na wapili ni kocha wa Benaco FC- James Elieza.
|
![]() |
|
Mwakilishi wa
Ligi ya Makoye -2014, Costantine Morandi akifatilia mchezo huo wa fainali March
30,2014,kati ya Benaco Stars na kumunazi FC katika uwanja wa Benaco-Ngara
,Kagera.
|
![]() |
|
Katika fainali hiyo ulinzi pia wakutosha uliimarishwa na askari mgambo na walinzi wa Polisi Jamii.
|
Magoli 2 ya
wachezaji Silvester John na Jacksoni John yalitosha kuwapa Ubingwa wa kwanza
msimu huu Timu ya Benaco Stars,baada ya hapo March 30,2014- Jumapili kufanikiwa
kuifunga timu ngumu ya Kumunazi FC bao 2-1.
Mchezo huo
uliokuwa wa fainali ya Ligi ya Makoye kwa timu za kata ya Kasulo,wilayani Ngara
mkoani Kagera,ulichezwa katika uwanja wa Benaco na kushuhudiwa na idadi kubwa
ya mashabiki na wapenzi wa soka toka katani humo.
Wakicheza
soka safi na la kuvutia ,licha ya uwanja kuwa na tope na kuteleza kwa sababu ya
mvua kunyesha kabla ya mchezo,Kumunazi FC walijikuta wakifungwa bao la kwanza
kwa njia ya Penati iliyofungwa na Jacksoni Joni baada ya mchezaji wa Kumunazi
ambae alikuwa wa mwisho kumkwatua rafu mchezaji wa Benaco FC katika eneo la
18,huku goli la kufutia machozi la Kumunazi FC likifungwa na Ramadhani Shija.
Baada ya
kumalizika mchezo ,kocha wa Benaco FC- James Elieza licha ya kufurahia Ubingwa
huo alitoa ushauri kwa kamati ya Mashindano ya Ligi ya Makoye,kuboresha mashindano yajayo kwa
kutatua changamoto mbalimbali zilizojitokeza za kisheria na Wamuuzi na kuzingatia kanuni za mashindano.
Kwa upande
wake Nahodha wa Timu ya Kumunazi FC-JUMA MUSSA licha ya kusifia mchezo huo wa
fainali kuwa mzuri lakini hakusita kuwatupia lawama mwamuzi wa kati wa mchezo
huo Ramadhani Makule,Rwegasira Kashunja na Abdul Mwandike kuwa hawakumudu vyema
sheria 17 zinazotawala mchezo wa soka.
Mshindi
katika fainali hiyo ya Ligi ya Makoye –Mfungaji bora alikuwa ni Ramadhani Shija
kwa kufunga magoli 9 toka timu ya Kumunazi FC -10,000,Timu yenye nidhamu
Kisabule FC-10,000-Washindi wa 3-Rusumo Sekondari-50,000-washindi wa pili
Kumunazi FC 100,000 na Mabingwa Benaco Starz
waliondoka na zawadi ya Ng'ombe mnyama mwenye thamani ya shilingi za
kitanzania Laki 5 na elfu 40 zawadi ambayo walikabidhiwa na Diwani wa kata ya
Kasulo Philbert Kiiza na kuwataka
kuitunza zawadi hiyo ili iwalete manufaa na kupiga hatua kiuchumi.
Awali kwa
niaba ya mdhamini wa Ligi ya Makoye-Athumani Makoye-mwakilishi wake Costantine
Morandi amesema kuwa mashindano hayo yatakuwa endelevu kwa kuchezwa kila Mwaka
katani humo.
Ligi hiyo
ilifadhiriwa na Athumani Makoye pamoja na mambo mengine alitoa vifaa vya
michezo kwa timu 8 zilizoshiriki vyevye thamani ya shilingi Milioni 4 na Laki 4
na elfu 80.



























No comments:
Post a Comment