BURUDANI:- Mwinjuma Muumini na Bendi yake ya Double M Sound watikisa Ngara…kwa Nyimbo-Fadhira kwa Wazazi na Shamba la BIBI. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Tuesday, April 22, 2014

demo-image

BURUDANI:- Mwinjuma Muumini na Bendi yake ya Double M Sound watikisa Ngara…kwa Nyimbo-Fadhira kwa Wazazi na Shamba la BIBI.

.com/simgad/
2014-04-22+00.45.00

Mkurugenzi wa Bendi ya Muziki wa Dansi ya Double M Sound Mwinjuma Muumini …akiimba wimbo wa fadhira kwa wazazi part two wakati huo akiwa na bendi ya Mchinga Sound..ndipo wazimu ulipompanda na kuamua kuvua….(wazimuuuu wangu ukinipanda…….hata nguo ntavuaaaa…..vuaaaa…nivue muoneeeee…….’’)Picha Na:-Seifu O.Upupu-Ngara.

2014-04-22+00.57.33

Mpiga gitaa wa bendi ya Double M Sound-Ally Akida aka Tetenasi ya Geneva akiungurumisha Jana (April 21,2014) wakati bendi hiyo ilipotumbuiza katika ukumbi wa New Happy mjini Ngara.
1

Kutoka Kushoto ni Seif Omary Upupu-ED-Chief Editor wa Radio Kwizeara akiwa na Mkurugenzi wa Bendi ya Double M Sound-Mwinjuma Muumini wakati alipofanya ziara ya kukitembelea Kituo cha Matangazo cha Radio Kwizera FM-Ngara pamoja na mambo mengi aliwaomba Wasikilizaji kumpigia kura kwa kuandika (SMS AC2 kisha tuma namba 15440).


Mkurugenzi wa Bendi ya Muziki wa Dansi ya Double M Sound Mwinjuma Muumini ameeleza namna alivyoupokea msiba wa Gwiji wa Muziki wa Dansi Nchini Muhidin Maalim Gurumo aliyefariki hivi karibuni jijini Dar es salaam na amesema kuwa kilichomsikitisha zaidi ni kuona Mzee Gurumo amefariki kabla hawajatimiza malengo yao ya kufanya kazi za pamoja kutokana na kukabiliwa na maradhi mfululizo.

Katika mahojiano na mwenzangu Seif Omary Upupu, Mwinjuma amesema Mzee Gurumo alikuwa akiwasaidia wanamuziki wengi katika ushauri wa masuala mbalimbaliu ya Kimuziki.

Pia akazungumzia ushiriki katika Tuzo za Muziki za Kilimanjaro ambzo zinahusisha wanamuziki wa aina mbalimbali, amewaomba Watanzania wote kumpigia kura katika Tuzo za mwaka za Kilimanjaro Music Award’s kwa kuchagua wimbo wake bora wa Kiswahili wa SHAMBA LA BIBI kwa kuandika (SMS AC2 kisha tuma namba 15440).

Baada ya miaka kadhaa ya ukimya wa Bendi yake ya Double M Sound aliyodai ilikufa kifo cha kawaida kutokana na uchakavu wa vifaa, Muumini amelazimika kukimbia jijini Dar Es Salaam na kuweka maskani mjini Kahama mkoani Shinyanga ambako ameifufua Bendi hiyo na kuahidi makubwa zaidi katika Bendi yake.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *