![]() |
|
Dr. Derick David ambaye ni Mkuu wa Idara ya Dharura Hospitali ya Rufaa
Bugando jijini Mwanza..Picha Na:-Gsengo.
|
Idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na ajali ya basi la kampuni ya Luhuye lililo
pata ajali April 21,2014,katika eneo la Masanza Kona Wilaya ya Busega Mkoani
Simiyu majira ya asubuhi likitokea wilayani Tarime Mkoani Mara Kwenda
Mwanza inatajwa kuongezeka kutoka ile ya awali 11 na sasa kufikia 16.
Kwa mujibu wa Dr. Derick David ambaye ni Mkuu wa Idara ya Dharura
Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza amesema kuwa jana(April 22,2014) idara
yake ilipokea watu 35, kati yao watu wawili walifariki dunia wakati wakipewa
matibabu, miili ya watu wengine wawili waliletwa ikiwa tayari imepoteza uhai
wakati wa harakati za kufikishwa hospitali hapo na mmoja ameongezeka akiwa
kwenye matibabu hivyo kufanya ongezeko la watu watano na kufikisha idadi ya
watu 16 hadi sasa.
![]() |
|
Ongezeko la majeruhi hospitalini hapo limesababisha msongamano kiasi cha kusababisha
wagonjwa kulazwa wawili wawili kwenye Kitanda kimoja.
|














No comments:
Post a Comment